EAGT PARADISE ni kanisa la Kipentekoste lililo chini ya EAGT, Kanisa hili lipo Mbagala Zakhem,karibu na viwanja vya wazi Zakhem(Kwa watengeneza masofa), PARADISE linaongozwa na Mtumishi wa Mungu Mchungaji Lugano Mwakisole.
Wednesday, July 16, 2014
Tuesday, July 15, 2014
Monday, July 14, 2014
UMUHIMU WA MABADILIKO
Nawasalimu kwa jina kuu la Yesu wasomaji wote wa Blog hii,
napenda kushiriki nanyi kile kilichofundishwa jana katika ibada,Tulipata mgeni kutoka Turiani Morogoro,Mtumishi wa Mungu Joshua Malundo yupo nasi kwa wiki ya pili sasa.
Anaendelea kutuletea yale mungu aliyompa kusema nasi.
Mungu alisema nasi juu ya UMUHIMU WA MABADILIKO,
Msingi wa somo hili ulitoka katika maandiko ya Mungu katika kitabu cha 1Samwel 10:1-7,
Kuna umuhimu mkubwa sana wa sisi kama watu wa Mungu kubadlika na hilo ndilo Mungu anatamani sana kuliona kutoka kwetu.Hata yeye alipotuokoa alitubadilisha kutoka kwenye utu wa kale na kutuvika utu upya.Lakini katika mabadiliko yapo yaliyo mbadiliko sahihi na ambayo si sahihi.
Badiliko linalotka kwa Mungu huwa ni sahihi sikuzote.Hitaji badiliko sahihi katika kila eneo la maisha yako.
Sehemu za picha katika ibada hiyo
kipindi cha Sifa |
Sehemu ya kusanyiko |
Mtumishi wa Mungu akitoa shukrani kwa kupata mtoto salama |
Mtumishi wa Mungu akimshukuru Mungu baada ya maombi yaliyofanyika kanisani hapa kwa wiki moja,Mungu ameanza kufungua njia katika kazi za mikono yake |
Mwenyekiti msaidizi wa ujenzi wa Hekalu la Mungu,naye alimshukuru Mungu kwa kumponya mguu wake uliovunjika wiki mbili zilizopita |
Baraka kutoka kwa Mchungaji |
Kwa Mungu wote ni vijana akimwimbia Mungu |
Mtumishi wa Mungu Teddy Komba |
Praise Team |
Tutamsifu Mungu kwa kila hali |
Mwinjilisti Joshua Malundo akifundisha |
Wakati wa Maombezi |
Darasa la watoto |
Saturday, July 5, 2014
SIKU 7 ZA MAOMBI YA KUFUNGA NA MKESHA ZAKARIBIA KUMALIZIKA
Ni neema nyingine ambayo Mungu Mwenye enzi ametupatia Paradise,
Mungu alisema na Mtumishi Wake Mchungaji Kiongozi Lugano Mwakisole juu ya maombi ya siku 7 kwa kanisa na juu ya ujenzi wa hema yake.
Maombi hayo yalianza Tar 30/06/2014 na yatamalizika tar 6/07/2014 Usiku.
Mungu ni wa ajabu sana kupitia maombi hayo kuna mambo mengi Mungu amefanya kwa mtu mmoja mmoja na kwa kanisa kwa ujumla.Tunaendelea kumtukuza Mungu maana ameonekana Paradise.
Hizi ni sehemu za Picha za wanajeshi wa Yesu walioshiriki katika mkesha huo.
Mungu alisema na Mtumishi Wake Mchungaji Kiongozi Lugano Mwakisole juu ya maombi ya siku 7 kwa kanisa na juu ya ujenzi wa hema yake.
Maombi hayo yalianza Tar 30/06/2014 na yatamalizika tar 6/07/2014 Usiku.
Mungu ni wa ajabu sana kupitia maombi hayo kuna mambo mengi Mungu amefanya kwa mtu mmoja mmoja na kwa kanisa kwa ujumla.Tunaendelea kumtukuza Mungu maana ameonekana Paradise.
Hizi ni sehemu za Picha za wanajeshi wa Yesu walioshiriki katika mkesha huo.