MCHUNGAJI LUGANO MWAKISOLE
AGANO JIPYA JUU YA ADUI ZETU.
(Math.5:43-47)
Leo
ninapenda tushirikishane mtazamo wa agano jipya juu ya adui zetu.
Mtazamo wa
agano la kale na agano jipya ni tofauti.Agano la kale(torati)kwa sehemu
linasema jino kwa jino au linaruhusu kulipa baya kwa baya lakini ni
tofauti na agano jipya linaagiza kuwatendea mema adui zetu.Si kwamba biblia
inapingana,kila watu walipewa maagizo na namna ya kuishi kwa wakati wake.sisi
tupo kipindi cha agano jipya na maagizo ya Yesu aliyoyatoa ni tofauti na ya
kale.
Maagizo tuliyopewa ni magumu zaidi na hii inatokana na pia tuna uwezo
mkubwa wa kushinda sababu tuna neema zaidi kutokana na ukombozi wa Yesu pia
tuna Roho Mtakatifu aliyemwagwa kwa wote tofauti na zamani ilikuwa kwa watu
maalumu.Daudi aliweza kusamehe na kumpenda adui yake sababu alikuwa na Roho
mtakatifu lakini ilikuwa ngumu kwa wafuasi wake kuelewa sababu walihishi kwa
sheria na kufuata maongozi ya Daudi lakini wenyewe hawakujazwa Roho.Tofauti na
sasa kila mtu amejaa Roho hivyo anawezeshwa kushinda vikwazo na kusamehe pia
kuwapenda adui kutokana na nguvu ya Roho mtakatifu iliyo ndani yetu.(waefeso
3;20)Si vema katika vipengele vigumu kukwepa maagizo ya agano jipya na kukimbilia
la kale ili kujifariji.Wengi wetu wanalipa kisasi na kujitetea kupitia maandiko
na wengine wanalaani na kutoa maneno ya laana pengine hata madhabahuni na
kutafuta maandiko ya kuwafariji.Biblia yapasa kuielewa kwa upana na kujifunza
kwa umakini,si kila andiko utalitumia kwa wakati huu.mengine yaweza kusomwa
kama historia au unabii uliopita,mengine ni ya sasa na yanahitaji kutekelezwa
na mengine ni unabii ujao yapasa uyajue lakini usitumie kwa sasa kama
utekelezaji utasababisha ajali katika uliwengu wa roho.Lakini yote tumewekewa
ili tujifunze na tukiyaelewa yatatufaa.
Mtazamo wa sasa juu ya adui zetu ni;
(a)kupenda adui zetu(mathayo 5;44)
Upendo wetu tunarithishwa na Yesu.aliwapenda adui hata siku
moja mbaya wake amebeba panga ili amkate Yesu,Petro akajibu mashambulizi kwa
kumkata sikio,lakini Yesu akamponya sikio lake na akamruhusu aendelee na ubaya
wake.(yohana 18:10 na luka22:50-51.)hili pendo ni la tofauti halifanani na
halielezeki,Na ndilo analotuagiza Bwana wetu Yesu Kristo kuwapenda adui zetu kwa kiasi hicho hata
wangepanga mabaya juu yako,wewe wapende,wakutengenezee kifo wewe wapende
tu.maisha yako ni mali ya Mungu hakuna anaweza kuchukua kama umesimama kwa
uaminifu kwa Mungu.
Mwenye kuhukumu ni Mungu tu na haki yako ipo mikononi mwake
usitumie nguvu kujitetea kama petro,mwachie yeye mwenye kuhukumu.
Maisha ya Yesu
ni kioo yapasa tuyaige.yeye hakupigana na adui kwa jinsi ya mwili nasi tufuate
mfano wake.Pia Paulo anazidi kusisitiza kuwa vita yetu ni ya ulimwengu wa
Roho(efeso 6:12)
(b)kubariki wanaotuudhi(warumi 12:14 na mathayo 5:44)
Tumeagizwa kubariki si kulaani,vinywa vyetu viponye.Watu wengine wanatumia mamlaka vibaya wengine utamka maneno ya laana katika madhabahu,hilo
ni kosa kubwa.Yesu walimdhihaki wakamnena mabaya mpaka msalabani jibu
alilosema"Baba uwasamehe hawajui watendalo",kipimo cha kujua kinywa cha
mkristo kimejaza nini ni wakati wa jaribu.Wengine wanatoa matusi,maneno ya
laana,lawama kuonyesha kuwa vinywa vimejaa uchafu.Bwana atakase kinywa chako
wakati wote.maneno yako yawe heri na baraka kwa wengine.
(c)kuwatendea mema wanaotuchukia.
Yesu akasema akunyang'anyae kanzu mpe na joho(mathayo
5;40).Mtendee mema adui yako,akiumwa mpeleke hospital,akiwa na njaa mpe chakula.
(d)kuwaombea wanaotuudhi na kututesa.
Kama Yesu alivyowaombea nasi tuige mfano wake.Tusiwatakie
mabaya lengo letu kubwa au ombi langu maadui zangu waokoke na wamjue Mungu
ninayemwabudu simpangii Bwana waokoke lini lakini najua ipo siku wataokoka.Na
Mungu ndiye aliyeumba mbaya na mwema na malipo ya
mbaya anayo yeye,namwachia mwenye kuhukumu.Tusishindwe na ubaya wala tusiwe na
kisasi(zab.34:13-14.)
TABIA NNE ZA MATENDO YA BINADAMU
(a)mtu akikutendea mabaya na ukalipa mabaya huo ni
ubinadamu(wanadamu wengi wanalipa baya kwa baya)
.(b)mtu akikutendea mema na ukalipa mabaya huo ni ushetani
au uibilisi.(atendaye hayo anakuwa amerithi tabia ya shetani)malipo ya shetani
hata ungemfurahisha kwa kumtumikia kwa nguvu mwisho wake ni kukuangamiza
tu hawezi hata siku moja akakulipa mema kusudi lake tangu mwanzo ni
kuua,kuchinja na kuharibu.Anaweza akakuvutia lakini hana nia njema ni kama mtu
anayefuga kuku wa nyama.atawahudumia vizuri kuku,anawapa chakula,madawa
wakiugua pengine kuku anaweza kuwaza huyu mtu ananipenda kumbe sivyo matokeo ya
mwisho ya hao kuku ni kuchinjwa tu.usifanye urafiki na shetani kuna siku
atakumaliza tu hata akufurahishe kuna siku atakuchinja.ACHANA NAYE KWA JINA LA
YESU.
(c)mtu akikutendea mabaya wewe ukalipa mema huo ni ukiUngu(
au hiyo ndiyo tabia ya KIMUNGU. Na ndivyo biblia inaagiza juu ya adui
zetu.atendaye hayo anapata thawabu kubwa kwa Mungu.Japo wanadamu wanaweza
kukuona mjinga lakini mbele za Mungu una maana kwa tendo hilo.
(d)ukitenda mema kwa mema huo ni ukiUngu au tabia apendayo
Mungu japo ni tabia ambayo wanadamu wengi utenda pia(haiwezi kufanana na ile ya
kulipa mema kwa aliyekutendea mabaya.kipimo cha mtu aliyeokoka kipo hapo na ni
wachache wanaoshinda.
Mchungaji:Lugano Mwakisole
EAGT Paradise Mbagala Zakhem
No comments:
Post a Comment
Andika maoni yako hapa
Note: Only a member of this blog may post a comment.