MATHAYO 4 :4 "mtu hataishi kwa mkate tu
bali kwakila neno litokalo katika kinywa
cha Mungu"
Wapendwa wasomaji napenda tushirikishane jambo kuu sana lina
lohusu baraka.kila mtu anapenda baraka lakini ni muhimu kufahamu msingi wa
baraka zetu tuliookoka unapatikana wapi,na wenzetu au mababa zetu wa Imani katika biblia
walipata baraka kupitia nini?soma zaidi upate kuelewa.
KUNA TOFAUTI YA KUFANIKIWA NA KUBARIKIWA.
Mafanikio ni matokeo ya mwilini bali baraka zinaanza rohoni
nakuonekana mwilini.Mtu aliyefanikiwa anaweza akawa na pesa,magari,majumba ya
kifahari(matokeo ya nje) lakini akawa hana amani,furaha ya ki Mungu na upendo wa
ki Mungu.pia ni mtu anayeishi kwa masharti mazito,na hofu tele juu ya utajiri
wake,hii tena si baraka bali ni mafanikio tu,baraka ni matokeo ya rohoni kwanza
inayobeba furaha,amani na upendo wa ki Mungu.Baraka inaanza rohoni kwa vitu
hivyo nilivyovitaja(upendo,furaha na amani ya kiMungu) ndipo inadhihirika
mwilini kama matokeo ya utajiri wa fedha,nyumba,magari nk.Mtu akipata vitu vya
mwilini akakosa amani na vitu hivyo au furaha ya Mungu anakuwa ni mtu wa
huzuni,anakosa upendo na ndugu zake au marafiki,mara nyingine anakuwa na ukali
usio na sababu, msongo wa mawazo japo ana kila kitu.Anapungukiwa na baraka au
vitu vya ndani (rohoni)vitakavyomfurahisha kwanza bali vinavyoonekana na
matokeo yake yanakuwa ni mabaya.Anaweza kuacha vyote na ukashangaa analala kwa
mganga wa kienyeji au mpunga pepo,katika mazingira machafu yasiyoendana na
yeye.tatizo alidhani baraka zinaanzia mwilini kumbe baraka zinaanza rohoni na
kumalizikia mwilini.maandiko yanasema"utafuteni kwanza ufalme wa Mungu na
haki zake na mengine tutazidishiwa"Haki zinazosemwa hapo ndio hizo furaha
amani pendo za kiMungu na mengine tunayozidishiwa ni utajiri tunaouona kama
fedha, magari,majumba n.k Na baraka zetu zinajengwa na neno la Mungu na huu
ndiyo msingi wetu.
Maisha yetu,kuishi kwetu,kula yetu,vaa
yetu na baraka zetu zimebebwa katika neno.
Na hii ndio maana ya kusema tunaishi kupitia
neno analosema Mungu.(math 4:4).Pia andiko la EBRANIA
10 : 38 linasema "mwenye haki wa mungu ataishi kwa imani"
inapoongelewa imani inamaanisha kusikia neno la kristo ,(WARUMI 10
:17) Hapo tunapata picha zaidi kuwa maisha yetu yote
na mafanikio yamebebwa na neno la Mungu:
Neno humjenga mtu katika imani na imani
inasababisha baraka zote za kimwili na kiroho.watu wengi wanapenda
kubarikwa lakini hawataki kuishi kwa neno,kulisoma neno,au kusikia
kupitia watumishi wa Mungu.Hawaendi kanisani kukutana na mtoa baraka kwa
kisingizio wana kazi nyingi. Ni vigumu watu hawa kupata baraka za
kiMungu.Baraka huja kupitia neno la Mungu, unapolisikia na kulitendea
kazi , na Baraka inaanzia rohoni ndipo hudhihirika
mwilini .Yohana aliandika waraka wake " 3YOHANA 1 :2 mpenzi naomba
ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na Afya njema kama vile roho yako
ifanikiwavyo" akiwa anamanisha baraka zote zinaanza rohoni
ndipo inadhihirika mwilini
MIFANO YA WATU WALIOBARIKIWA KUPITIA NENO LA MUNGU.
1. Ibrahimu baba wa imani(MWANZO 12:1-3)
Ibrahimu aliambiwa neno na Mungu atoke aende katika
nchi ambayo aliandaliwa baraka tele.
Baraka zilianza pale tu Ibrahimu alipotii neno au agizo na
akatekeleza.mstari wa 4 ibrahim alitekeleza na alipotoka baraka zilimfuata kama
neno liliivyomwambia.japo alipitia mitihani mingi lakini ushindi wa mwisho
ulikuwa mkuu sana na matokeo yake ni makubwa,Tunaona matokeo ya taifa la israel
ni kutokana na kutii kwa ibrahim.ishi kwa neno na kutii kama Ibrahim utaziona
baraka kwako na familia yako na hata kizazi chako chote.
2 NABII ELIYA: WAFALME 17 :1-16
Hapo tunaona maisha alioishi Eliya baada ya kutokea njaa iliyosababishwa na maombi yake mwenyewe. Baada ya kuzuia mvua kulikuwa na ukame na njaa kubwa katika mji wa israeli wakati huo mgumu watu wengi walisumbuka sana kutafuta chakula lakini Eliya kwake maisha hayakuwa magumu sababu yeye aliishi kwa neno la Mungu.
Hapo tunaona maisha alioishi Eliya baada ya kutokea njaa iliyosababishwa na maombi yake mwenyewe. Baada ya kuzuia mvua kulikuwa na ukame na njaa kubwa katika mji wa israeli wakati huo mgumu watu wengi walisumbuka sana kutafuta chakula lakini Eliya kwake maisha hayakuwa magumu sababu yeye aliishi kwa neno la Mungu.
Ukisoma mstari 2-7 Neno lilimjia Eliya
aende katika kijito cha kerithi. Alipotii kwenda huko Mungu
alikuwa amemwandalia kunguru wamlishe katika kijito hicho na kunywa
maji hayo. wakati huo mgumu , Eliya haukumsumbua kwasababu
yeye alitii neno la Bwana na aliweza kuishi.Hali ngumu za maisha au
kukosa pesa si sababu ya kukata tamaa kwani tukiamini neno lake,Mungu atafungua
njia juu yetu.kumbuka neno linasema "dunia na vyote viijazavyo ni mali ya
Bwana,ZABURI 24:1.Pia anatupa ahadi kuwa tukimwomba yeye atatupa kwa kuwa na
sisi ni watoto wake.(MATH 7:7-11)
Mstari 8:16 katika 1wafalme 17 tumeona kijito
kilikauka kutokana na hali ya ukame, lakini hilo
halikumtisha Eliya bali alisikiliza maelekezo ya neno.
Ndipo neno likamwongoza kwenda kwa mwanamke mjane wa serepta na akafanya
muujiza kupitia mafuta kidogo katika chupa na unga kidogo. Na muujiza
mkubwa ukafanyika wakaishi.
Eliya hakutishwa na mabadiliko ya hali ya hewa
bali aliamini neno kuwa litamfanya aishi . Je ni kitu gani kinakufanya
uwe na hofu ya maisha, je kukosa kazi, mabadiliko ya uchumi, au kukataliwa na
ndugu au jamaa.? Vyote hivyo haviwezi kuzuia baraka zetu sababu sisi hatuishi
kwa bahati(hatubahatishi maisha) bali maisha yetu yanaongozwa na
neno (MATHAYO 4:4).Watu wasiookoka wanaishi kwa bahati na ndio maana wanaishi
kwa wasiwasi na wengine husema "bahati hairudi mara mbili"sababu
wanabahatisha wanakuwa na hofu wakifilisika utakuwa ndio mwisho wao.Sisi
tuliookoka tunaishi kwa neno au maongozi ya neno na baraka zetu ni nyingi hata
zikizuiliwa na shetani au watu wenye hila sehemu fulani,iwe kufukuzwa
kazi,kudhurumiwa,kutendewa mabaya na watu tuliowaamini lakini
wakageuka,bado Mungu atafungua kwa njia nyingine. Sisi ni wabarikiwa na ni
kipawa tulichopewa kama biblia isemavyo"kipawa ni kito cha thamani na kila
kigeukapo hufanikiwa,)Maana ya kila kigeukapo inamaanisha kila uendapo na kila
ufanyacho utafanikiwa.Shetani japo alijaribu kugusa maisha ya Ayubu kwa
magonjwa,kuuwa watoto wake na mifugo na mali zake kufilisiiwa,bado alimtegemea
Mungu na matokeo ya mwisho yalikuwa mazuri kuliko mwanzo na alipata utajiri
mwingi kuliko mwanzo.Hata kama shetani alichezea uchumi wako na ukakata
tamaa,nakutia moyo kuwa baraka yako bado ipo si za kubahatisha,Yesu atakubariki
kwani anazo baraka nyingi.Pia baraka zetu zinatufuata popote tunapoenda kama
neno lisemavyo " hakika wema na fadhiri zitatufuata siku zote
za maisha yetu, ZABUR 23:6"
Pia baraka zetu anayetoa ni Mungu na ndie anatupa nguvu za
kupata utajiri( KUMB 8:17:18) Wala si uwezo wetu hivyo tumtegemee
yeye ambae ndiye neno (YOHAN 1:1) Ili atupe mahitaji yetu,
Vitu vyote vipo chini yake na anatoa kwakila mtu anaye
mcha na kumtii( 1MAMB NYKT 29:12).
Ushauri wangu kwako mpe Yesu maisha yako utapata baraka za Bwana ambazo zinajumuishwa na upendo,furaha,na amani kisha utajiri wa fedha,mifugo,mashamba,majumba,magari n.k Bwana atatuzidishia na baraka ya Mungu inaenda hatua kwa hatua,yapasa uwe mvumilivu kama baba yetu Ibrahim aliyepita wakati mgumu lakini mwisho wake ulikuwa mzuri.Usitake utajiri kwa haraka dunia itakupoteza.wengi tunawaona walitaka utajiri kwa haraka lakini wamekufa mapema tena kwa vifo vya kuhuzunisha na pesa na utajiri wao hawakuufaidi bali wamefaidika wengine.Baraka ya Mungu hutajirisha na haichangamani na majuto.Mungu awabariki.
Kwa Msaada Zaidi
Waweza kuwasiliana nami
0688387834
luggymakky@gmail.com
Ushauri wangu kwako mpe Yesu maisha yako utapata baraka za Bwana ambazo zinajumuishwa na upendo,furaha,na amani kisha utajiri wa fedha,mifugo,mashamba,majumba,magari n.k Bwana atatuzidishia na baraka ya Mungu inaenda hatua kwa hatua,yapasa uwe mvumilivu kama baba yetu Ibrahim aliyepita wakati mgumu lakini mwisho wake ulikuwa mzuri.Usitake utajiri kwa haraka dunia itakupoteza.wengi tunawaona walitaka utajiri kwa haraka lakini wamekufa mapema tena kwa vifo vya kuhuzunisha na pesa na utajiri wao hawakuufaidi bali wamefaidika wengine.Baraka ya Mungu hutajirisha na haichangamani na majuto.Mungu awabariki.
Kwa Msaada Zaidi
Waweza kuwasiliana nami
0688387834
luggymakky@gmail.com
No comments:
Post a Comment
Andika maoni yako hapa
Note: Only a member of this blog may post a comment.