MCHUNGAJI LUGANO MWAKISOLE |
KUWA RAFIKI WA KARIBU WA YESU
Kuna utofauti mkubwa kuwa
rafiki na mwanafunzi,
Kuwa rafiki wa Yesu ni zaidi
ya kuwa mwanafunzi wake,Ni kiwango ambacho si rahisi kwa mwamini kufikia kuwa
rafiki wa Karibu wa Yesu,Ni hatua ya juu sana
Ukiwa rafiki wa Yesu unapata
nafasi ya kuongaea na nae ana kwa ana,
Katika Somo hili tutajifunza
Jinsi Gani sisi kama wanafunzi wa Yesu tunaweza kuwa Rafiki zake wa
karibu.Fuata nami na Mungu atakubariki
HATUA ZA KUWA RAFIKI WA YESU.
1.UTII
hatua hii ni ya muhimu sana
ili ufikie kuwa rafiki.Yesu amesema ninyi mmekuwa rafiki zangu mkitenda
niwaamuruyo(Yohana 15:14),Yesu anathibitisha kuwa ili tuwe marafiki zake ni
lazima tutii maagizo yake..kipimo cha kumpenda Yesu ni kutii maagizo
yake.pia katika Yohana 14:21 inasema "Yeye aliye na amri zangu, na
kuzishika,yeye ndiye anipendaye;naye anipendaye atapendwa na Baba yangu,nami
nitampenda na kujidhihirisha kwake" mtu anayeshika amri au maagizo ya Yesu
ndiye ependwaye na Yesu au anakuwa rafiki wa Yesu.Yesu alimuuliza Petro mara
tatu kama kweli anampenda.(Yohana 21:15-17),Petro alipojitetea kwa sababu
nyingi na kutaka kuonyesha kuwa anampenda Yesu alimjibu kuwa achunge na kulisha
kundi.Kumbuka alimuuliza maswali haya baada ya kufufuka akisikitishwa na Petro
kuacha kutii wito aliomwachia kabla ya kufa na malezi yote aliyompa kwa
muda wote aliokaa naye.pia alipomwita aliwambia aache kuvua samaki naye
atamfanya kuwa mvuvi wa watu.Muda mfupi tu Yesu alipomwacha ameacha kutii agizo
ameenda kuvua samaki.kitendo cha kutokutii wito Yesu akahuzunika sana na
kumuuliza kweli anampenda? Tatizo ni kutokutii ndicho Yesu kilichomsononesha.Pia
lazima tujiulize mbona anaulizwa Petro si wanafunzi wengine?wakati kwenye kuvua
samaki walikuwa wengi,Jibu ni hili Yesu hakutegemea rafiki yake mpendwa au mwanafunzi
wa karibu zaidi ndio kaharibu.Ukiwa rafiki wa Yesu ni lazima uwe na utii wa hali
ya juu katika maagizo ndipo Yesu atakuwa na imani nawe.usifanye kitu
kitakachosababisha Yesu kuwa na mashaka na urafiki wenu kama Petro.Mimi na wewe
tujiulize je tumesimamia wito wetu na kutii kila agizo ili Yesu atupende
kama rafiki zake?
2.KUPENDA KUJIFUNZA
Hii ni hatua ya muhimu na
Yesu anaizingatia sana kwa marafiki zake.(Yohana 8:31) Yesu anasema “ninyi
mkishika neno langu mmekuwa wanafunzi wangu kwelikweli” kuwa mwanafunzi
kwelikweli kwa maana nyingine ni kuwa mwanafunzi anayepita wanafunzi wengine au
kuwa rafiki wa karibu.Tuna mfano wa dada aliyekuwa rafiki sana wa Yesu anaitwa
Mariam.alikaa miguuni pa Yesu akijifunza.(luka 10:38-42) Yesu alimpenda na
akasema amechagua fungu jema,na kihistoria anaonyesha ni miongoni mwa rafiki wa
karibu wa Yesu.Sehemu nyingi zinaonyesha kama kufa kwake,kufufuka kwake,na mpaka
anapaa alikuwa karibu naye sana.
3.HATUA YA UTOAJI
Hii ni sadaka ya tofauti na sadaka
ya kawaida.sadaka ambayo inamgusa Yesu kwa kiwango cha juu.Sadaka ambayo Yesu
akiangalia inamkumbusha sadaka yake kubwa aliyoitoa msalabani.ukitoa sadaka ya
namna hiyo ni lazima Yesu awe rafiki yako.sadaka hiyo inakufanya wewe
uchukuliwe uwe karibu na sadaka ya msalaba.Watu wengi waliotoa kwa kiwango cha
juu kama hicho waliugusa moyo wa Yesu na kuwa marafiki zake.
-Mfano wa kwanza ni baba wa
imani Ibrahim alikubali kumtoa mwanawe wa pekee Isaka kuwa sadaka ya
kuteketezwa.kitendo cha kutoa mtoto wa pekee ,mpendwa,kilimkumbusha Mungu
kumtoa mwanawe wa pekee Yesu kufa msalabani. Unaweza kusema mbona wakati huo
Yesu alikuwa bado hajafa.kumbuka mpango wa Yesu kufa ulipangwa na Mungu zamani
sana biblia inasema kabla ya kuwekwa misingi ya dunia(1petro1:19-20) kwahiyo
utoaji wa Ibrahim ulikuwa utabiri wa Yesu na ulimfanya Ibrahim kumkumbusha
Mungu sadaka yake.habari yote unaipata katika kitabu cha mwanzo 22.sura
yote.Pia tunaona katika msitari wa 11-12 malaika wa Bwana anamsifia Ibrahim kwa
moyo wake wa kumcha Bwana.Mungu aliuona moyo wa Ibrahim baada ya kutoa sadaka
ya tofauti.urafiki wa MUNGU na Ibrahim uliongezeka.
Mstari wa 13 Mungu
anatoa kondoo badala ya Isaka,hapa inafundisha kuwa yeyote atakayetoa kwa kiwango
cha juu na sadaka ya pekee,maalumu au inayogusa moyo wake Mungu lazima atoe
mbadala kwa lugha nyingine Mungu atakulipa kwa njia tofauti kama Ibrahim
alivyolipwa
(mst 15-18)
-Mfano mwingine ni Mariam Magdalena.pamoja
na kukaa miguuni pa Yesu na kujifunza lakini pia alimtegemeza Yesu kwa mali
zake.kuna sadaka moja ilimgusa Yesu,alipompaka Yesu kwa mafuta ya
thamani.katika desturi ya wayahud kulikuwa na kutawadha miguu na hii ilikuwa kwa
mtumwa kutawadha Bwana wake.Mariam hakutumia kitambaa,yeye akatumia
nywele za kichwa chake,pia wengine walitumia maji lakini yeye alitumia machozi
yake na mafuta ya thamani.(Yohana 12:3 na luka7:36-38)kitendo hiki kiligusa
moyo wa Yesu na kilimshangaza,mafuta thamani kubwa kumtawadha Yesu,ni sadaka kubwa
sana alitoa.Unyenyekevu wa Mariam(kudondosha machozi ishara ya maombi na
kumfuta kwa nywele zake kuonyesha kushuka),sadaka yake kubwa(kitendo cha
kutojari mali zake kwaajili ya Yesu)na kupenda kukaa miguuni pa Yesu na
kujifunza kilifanya Yesu awe rafiki yake zaidi ya wanafunzi wengine.
Bado kuna hatua nyingine tatu
ili kukamilisha kuwa rafiki wa Yesu,tutaendelea nazo wiki ijayo siku kama
hii.Ombi langu tafuta kuwa rafiki wa Yesu utapata faida nyingi ambazo
utazifahamu utakapoendelea na somo mpaka mwisho.
MUNGU AWABARIKI.
Mchungaji:Lugano Mwakisole
EAGT Paradise Mbagala Zakhem
No comments:
Post a Comment
Andika maoni yako hapa
Note: Only a member of this blog may post a comment.