Wednesday, August 27, 2014

KUWA RAFIKI WA KARIBU WA YESU-Mch.Lugano Mwakisole

MCHUNGAJI LUGANO MWAKISOLE

KUWA RAFIKI WA KARIBU WA YESU
Kuna utofauti mkubwa kuwa rafiki na mwanafunzi,
Kuwa rafiki wa Yesu ni zaidi ya kuwa mwanafunzi wake,Ni kiwango ambacho si rahisi kwa mwamini kufikia kuwa rafiki wa Karibu wa Yesu,Ni hatua ya juu sana
Ukiwa rafiki wa Yesu unapata nafasi ya kuongaea na nae ana kwa ana,
Katika Somo hili tutajifunza Jinsi Gani sisi kama wanafunzi wa Yesu tunaweza kuwa Rafiki zake wa karibu.Fuata nami na Mungu atakubariki

HATUA ZA KUWA RAFIKI WA YESU.
1.UTII
hatua hii ni ya muhimu sana ili ufikie kuwa rafiki.Yesu amesema ninyi mmekuwa rafiki zangu mkitenda niwaamuruyo(Yohana 15:14),Yesu anathibitisha kuwa ili tuwe marafiki zake ni lazima tutii maagizo yake..kipimo cha  kumpenda Yesu ni kutii maagizo yake.pia katika Yohana 14:21 inasema "Yeye aliye na amri zangu, na kuzishika,yeye ndiye anipendaye;naye anipendaye atapendwa na Baba yangu,nami nitampenda na kujidhihirisha kwake" mtu anayeshika amri au maagizo ya Yesu ndiye ependwaye na Yesu au anakuwa rafiki wa Yesu.Yesu alimuuliza Petro mara tatu kama kweli anampenda.(Yohana 21:15-17),Petro alipojitetea kwa sababu nyingi na kutaka kuonyesha kuwa anampenda Yesu alimjibu kuwa achunge na kulisha kundi.Kumbuka alimuuliza maswali haya baada ya kufufuka akisikitishwa na Petro kuacha kutii wito aliomwachia kabla ya kufa  na malezi yote aliyompa kwa muda wote aliokaa naye.pia alipomwita aliwambia aache kuvua samaki naye atamfanya kuwa mvuvi wa watu.Muda mfupi tu Yesu alipomwacha ameacha kutii agizo ameenda kuvua samaki.kitendo cha kutokutii wito Yesu akahuzunika sana na kumuuliza kweli anampenda? Tatizo ni kutokutii ndicho Yesu kilichomsononesha.Pia lazima tujiulize mbona anaulizwa Petro si wanafunzi wengine?wakati kwenye kuvua samaki walikuwa wengi,Jibu ni hili Yesu hakutegemea rafiki yake mpendwa au mwanafunzi wa karibu zaidi ndio kaharibu.Ukiwa rafiki wa Yesu ni lazima uwe na utii wa hali ya juu katika maagizo ndipo Yesu atakuwa na imani  nawe.usifanye kitu kitakachosababisha Yesu kuwa na mashaka na urafiki wenu kama Petro.Mimi na wewe tujiulize je tumesimamia wito wetu na kutii kila agizo ili  Yesu atupende kama rafiki zake?

2.KUPENDA KUJIFUNZA
Hii ni hatua ya muhimu na Yesu anaizingatia sana kwa marafiki zake.(Yohana 8:31) Yesu anasema “ninyi mkishika neno langu mmekuwa wanafunzi wangu kwelikweli” kuwa mwanafunzi kwelikweli kwa maana nyingine ni kuwa mwanafunzi anayepita wanafunzi wengine au kuwa rafiki wa karibu.Tuna mfano wa dada aliyekuwa rafiki sana wa Yesu anaitwa Mariam.alikaa miguuni pa Yesu akijifunza.(luka 10:38-42) Yesu alimpenda na akasema amechagua fungu jema,na kihistoria anaonyesha ni miongoni mwa rafiki wa karibu wa Yesu.Sehemu nyingi zinaonyesha kama kufa kwake,kufufuka kwake,na mpaka anapaa alikuwa karibu naye sana.


3.HATUA YA UTOAJI
Hii ni sadaka ya tofauti na sadaka ya kawaida.sadaka ambayo inamgusa Yesu kwa kiwango cha juu.Sadaka ambayo Yesu akiangalia inamkumbusha sadaka yake kubwa aliyoitoa msalabani.ukitoa sadaka ya namna hiyo ni lazima Yesu awe rafiki yako.sadaka hiyo inakufanya wewe uchukuliwe uwe karibu na sadaka ya msalaba.Watu wengi waliotoa kwa kiwango cha juu kama hicho waliugusa moyo wa Yesu na kuwa marafiki zake.
-Mfano wa kwanza ni baba wa imani Ibrahim alikubali kumtoa mwanawe wa pekee  Isaka kuwa sadaka ya kuteketezwa.kitendo cha kutoa mtoto wa pekee ,mpendwa,kilimkumbusha Mungu kumtoa mwanawe wa pekee Yesu kufa msalabani. Unaweza kusema mbona wakati huo Yesu alikuwa bado hajafa.kumbuka mpango wa Yesu kufa ulipangwa na Mungu zamani sana biblia inasema kabla ya kuwekwa misingi ya dunia(1petro1:19-20) kwahiyo utoaji wa Ibrahim ulikuwa utabiri wa Yesu na ulimfanya Ibrahim kumkumbusha Mungu sadaka yake.habari yote unaipata katika kitabu cha mwanzo 22.sura yote.Pia tunaona katika msitari wa 11-12 malaika wa Bwana anamsifia Ibrahim kwa moyo wake wa kumcha Bwana.Mungu aliuona moyo wa Ibrahim baada ya kutoa sadaka ya tofauti.urafiki wa MUNGU na Ibrahim uliongezeka.
 Mstari wa 13 Mungu anatoa kondoo badala ya Isaka,hapa inafundisha kuwa yeyote atakayetoa kwa kiwango cha juu na sadaka ya pekee,maalumu au inayogusa moyo wake Mungu lazima atoe mbadala kwa lugha nyingine Mungu atakulipa kwa njia tofauti kama Ibrahim alivyolipwa
(mst 15-18)

-Mfano mwingine ni Mariam Magdalena.pamoja na kukaa miguuni pa Yesu na kujifunza lakini pia alimtegemeza Yesu kwa mali zake.kuna sadaka moja ilimgusa Yesu,alipompaka Yesu kwa mafuta ya thamani.katika desturi ya wayahud kulikuwa na kutawadha miguu na hii ilikuwa kwa mtumwa kutawadha Bwana wake.Mariam hakutumia kitambaa,yeye  akatumia nywele za kichwa chake,pia wengine walitumia maji lakini yeye alitumia machozi yake na mafuta ya thamani.(Yohana 12:3 na luka7:36-38)kitendo hiki kiligusa moyo wa Yesu na kilimshangaza,mafuta thamani kubwa kumtawadha Yesu,ni sadaka kubwa sana alitoa.Unyenyekevu wa Mariam(kudondosha machozi ishara ya maombi na kumfuta kwa nywele zake kuonyesha kushuka),sadaka yake kubwa(kitendo cha kutojari mali zake kwaajili ya Yesu)na kupenda kukaa miguuni pa Yesu na kujifunza kilifanya Yesu awe rafiki yake zaidi ya wanafunzi wengine.

Bado kuna hatua nyingine tatu ili kukamilisha kuwa rafiki wa Yesu,tutaendelea nazo wiki ijayo siku kama hii.Ombi langu tafuta kuwa rafiki wa Yesu utapata faida nyingi ambazo utazifahamu utakapoendelea na somo mpaka mwisho.
MUNGU AWABARIKI.


Mchungaji:Lugano Mwakisole

EAGT Paradise Mbagala Zakhem




No comments:

Post a Comment

Andika maoni yako hapa

Note: Only a member of this blog may post a comment.