Sunday, August 31, 2014

Ibada ya Leo Jumapili EAGT Paradise Church

Ibada ya Leo Jumapili EAGT Paradise Church

by Eagt Paradise



August 31, 2014 at 09:43PM

from Facebook

via IFTTTfrom Facebook

via IFTTT

Ni Siku njema ambayo Bwana ametupa,baada ya Siku Sita za kufanya kazi Leo itenge iwe Siku ya kumfanyia Bwana Ibada.

Ni Siku njema ambayo Bwana ametupa,baada ya Siku Sita za kufanya kazi Leo itenge iwe Siku ya kumfanyia Bwana Ibada.

by Eagt Paradise



August 31, 2014 at 10:06AM

from Facebook

via IFTTTfrom Facebook

via IFTTT

Wednesday, August 27, 2014

KUWA RAFIKI WA KARIBU WA YESU-Mch.Lugano Mwakisole

MCHUNGAJI LUGANO MWAKISOLE

KUWA RAFIKI WA KARIBU WA YESU
Kuna utofauti mkubwa kuwa rafiki na mwanafunzi,
Kuwa rafiki wa Yesu ni zaidi ya kuwa mwanafunzi wake,Ni kiwango ambacho si rahisi kwa mwamini kufikia kuwa rafiki wa Karibu wa Yesu,Ni hatua ya juu sana
Ukiwa rafiki wa Yesu unapata nafasi ya kuongaea na nae ana kwa ana,
Katika Somo hili tutajifunza Jinsi Gani sisi kama wanafunzi wa Yesu tunaweza kuwa Rafiki zake wa karibu.Fuata nami na Mungu atakubariki

HATUA ZA KUWA RAFIKI WA YESU.
1.UTII
hatua hii ni ya muhimu sana ili ufikie kuwa rafiki.Yesu amesema ninyi mmekuwa rafiki zangu mkitenda niwaamuruyo(Yohana 15:14),Yesu anathibitisha kuwa ili tuwe marafiki zake ni lazima tutii maagizo yake..kipimo cha  kumpenda Yesu ni kutii maagizo yake.pia katika Yohana 14:21 inasema "Yeye aliye na amri zangu, na kuzishika,yeye ndiye anipendaye;naye anipendaye atapendwa na Baba yangu,nami nitampenda na kujidhihirisha kwake" mtu anayeshika amri au maagizo ya Yesu ndiye ependwaye na Yesu au anakuwa rafiki wa Yesu.Yesu alimuuliza Petro mara tatu kama kweli anampenda.(Yohana 21:15-17),Petro alipojitetea kwa sababu nyingi na kutaka kuonyesha kuwa anampenda Yesu alimjibu kuwa achunge na kulisha kundi.Kumbuka alimuuliza maswali haya baada ya kufufuka akisikitishwa na Petro kuacha kutii wito aliomwachia kabla ya kufa  na malezi yote aliyompa kwa muda wote aliokaa naye.pia alipomwita aliwambia aache kuvua samaki naye atamfanya kuwa mvuvi wa watu.Muda mfupi tu Yesu alipomwacha ameacha kutii agizo ameenda kuvua samaki.kitendo cha kutokutii wito Yesu akahuzunika sana na kumuuliza kweli anampenda? Tatizo ni kutokutii ndicho Yesu kilichomsononesha.Pia lazima tujiulize mbona anaulizwa Petro si wanafunzi wengine?wakati kwenye kuvua samaki walikuwa wengi,Jibu ni hili Yesu hakutegemea rafiki yake mpendwa au mwanafunzi wa karibu zaidi ndio kaharibu.Ukiwa rafiki wa Yesu ni lazima uwe na utii wa hali ya juu katika maagizo ndipo Yesu atakuwa na imani  nawe.usifanye kitu kitakachosababisha Yesu kuwa na mashaka na urafiki wenu kama Petro.Mimi na wewe tujiulize je tumesimamia wito wetu na kutii kila agizo ili  Yesu atupende kama rafiki zake?

2.KUPENDA KUJIFUNZA
Hii ni hatua ya muhimu na Yesu anaizingatia sana kwa marafiki zake.(Yohana 8:31) Yesu anasema “ninyi mkishika neno langu mmekuwa wanafunzi wangu kwelikweli” kuwa mwanafunzi kwelikweli kwa maana nyingine ni kuwa mwanafunzi anayepita wanafunzi wengine au kuwa rafiki wa karibu.Tuna mfano wa dada aliyekuwa rafiki sana wa Yesu anaitwa Mariam.alikaa miguuni pa Yesu akijifunza.(luka 10:38-42) Yesu alimpenda na akasema amechagua fungu jema,na kihistoria anaonyesha ni miongoni mwa rafiki wa karibu wa Yesu.Sehemu nyingi zinaonyesha kama kufa kwake,kufufuka kwake,na mpaka anapaa alikuwa karibu naye sana.


3.HATUA YA UTOAJI
Hii ni sadaka ya tofauti na sadaka ya kawaida.sadaka ambayo inamgusa Yesu kwa kiwango cha juu.Sadaka ambayo Yesu akiangalia inamkumbusha sadaka yake kubwa aliyoitoa msalabani.ukitoa sadaka ya namna hiyo ni lazima Yesu awe rafiki yako.sadaka hiyo inakufanya wewe uchukuliwe uwe karibu na sadaka ya msalaba.Watu wengi waliotoa kwa kiwango cha juu kama hicho waliugusa moyo wa Yesu na kuwa marafiki zake.
-Mfano wa kwanza ni baba wa imani Ibrahim alikubali kumtoa mwanawe wa pekee  Isaka kuwa sadaka ya kuteketezwa.kitendo cha kutoa mtoto wa pekee ,mpendwa,kilimkumbusha Mungu kumtoa mwanawe wa pekee Yesu kufa msalabani. Unaweza kusema mbona wakati huo Yesu alikuwa bado hajafa.kumbuka mpango wa Yesu kufa ulipangwa na Mungu zamani sana biblia inasema kabla ya kuwekwa misingi ya dunia(1petro1:19-20) kwahiyo utoaji wa Ibrahim ulikuwa utabiri wa Yesu na ulimfanya Ibrahim kumkumbusha Mungu sadaka yake.habari yote unaipata katika kitabu cha mwanzo 22.sura yote.Pia tunaona katika msitari wa 11-12 malaika wa Bwana anamsifia Ibrahim kwa moyo wake wa kumcha Bwana.Mungu aliuona moyo wa Ibrahim baada ya kutoa sadaka ya tofauti.urafiki wa MUNGU na Ibrahim uliongezeka.
 Mstari wa 13 Mungu anatoa kondoo badala ya Isaka,hapa inafundisha kuwa yeyote atakayetoa kwa kiwango cha juu na sadaka ya pekee,maalumu au inayogusa moyo wake Mungu lazima atoe mbadala kwa lugha nyingine Mungu atakulipa kwa njia tofauti kama Ibrahim alivyolipwa
(mst 15-18)

-Mfano mwingine ni Mariam Magdalena.pamoja na kukaa miguuni pa Yesu na kujifunza lakini pia alimtegemeza Yesu kwa mali zake.kuna sadaka moja ilimgusa Yesu,alipompaka Yesu kwa mafuta ya thamani.katika desturi ya wayahud kulikuwa na kutawadha miguu na hii ilikuwa kwa mtumwa kutawadha Bwana wake.Mariam hakutumia kitambaa,yeye  akatumia nywele za kichwa chake,pia wengine walitumia maji lakini yeye alitumia machozi yake na mafuta ya thamani.(Yohana 12:3 na luka7:36-38)kitendo hiki kiligusa moyo wa Yesu na kilimshangaza,mafuta thamani kubwa kumtawadha Yesu,ni sadaka kubwa sana alitoa.Unyenyekevu wa Mariam(kudondosha machozi ishara ya maombi na kumfuta kwa nywele zake kuonyesha kushuka),sadaka yake kubwa(kitendo cha kutojari mali zake kwaajili ya Yesu)na kupenda kukaa miguuni pa Yesu na kujifunza kilifanya Yesu awe rafiki yake zaidi ya wanafunzi wengine.

Bado kuna hatua nyingine tatu ili kukamilisha kuwa rafiki wa Yesu,tutaendelea nazo wiki ijayo siku kama hii.Ombi langu tafuta kuwa rafiki wa Yesu utapata faida nyingi ambazo utazifahamu utakapoendelea na somo mpaka mwisho.
MUNGU AWABARIKI.


Mchungaji:Lugano Mwakisole

EAGT Paradise Mbagala Zakhem




Monday, August 25, 2014

Naibariki Jumanne yako,Mungu akupe kibali Kwa kila lililo Mbele yako Kwa Jina la Yesu

Naibariki Jumanne yako,Mungu akupe kibali Kwa kila lililo Mbele yako Kwa Jina la Yesu

by Eagt Paradise



August 26, 2014 at 08:28AM

from Facebook

via IFTTTfrom Facebook

via IFTTT

MAFUNDISHO:MAMBO YA NGUVU YAKUFUATE-Mch.MATHAYO HENRY

KUWA RAFIKI WA KARIBU NA YESU

IBADA YA JUMAPILI 24.8.2014 KATIKA PICHA

Mtumishi wa Mungu Majaliwa akimtukuza Mungu kwa wimbio wake "KWA MSAADA WA ROHO"

Mama Mchungaji akimtumikia Mungu kwa njia ya Uimbaji



Kwaya ya Kanisa ikihudumu

Kwaya ya Kanisa ikihudumu

Kwaya ya Kanisa ikihudumu

Kwaya ya Kanisa ikihudumu

Kwaya ya Kanisa ikihudumu

Mzee wa Kanisa Shedrack 



Mtumishi wa Mungu,Mch.Lugano Mwakisole akileta kusudi la Mungu kwa Kusanyiko


Wakati wa Maombezi

Wednesday, August 20, 2014

Dhambi ina matokeo mabaya http://ift.tt/1n8WRXN

Dhambi ina matokeo mabaya http://ift.tt/1n8WRXN

by Eagt Paradise



August 20, 2014 at 12:30PM

from Facebook

via IFTTTfrom Facebook

via IFTTT

Tuesday, August 19, 2014

AGANO JIPYA JUU YA ADUI ZETU-Mch.Lugano Mwakisole


MCHUNGAJI LUGANO MWAKISOLE

AGANO JIPYA JUU YA  ADUI ZETU.
(Math.5:43-47)

Leo ninapenda tushirikishane mtazamo wa agano jipya juu ya adui zetu.
Mtazamo wa agano la kale na agano jipya ni tofauti.Agano la kale(torati)kwa sehemu linasema  jino kwa jino au linaruhusu kulipa baya kwa baya lakini ni tofauti na agano jipya linaagiza kuwatendea mema adui zetu.Si kwamba biblia inapingana,kila watu walipewa maagizo na namna ya kuishi kwa wakati wake.sisi tupo kipindi cha agano jipya na maagizo ya Yesu aliyoyatoa ni tofauti na ya kale.

Maagizo tuliyopewa ni magumu zaidi na hii inatokana na pia tuna uwezo mkubwa wa kushinda sababu tuna neema zaidi kutokana na ukombozi wa Yesu pia tuna Roho Mtakatifu aliyemwagwa kwa wote tofauti na zamani ilikuwa kwa watu maalumu.Daudi aliweza kusamehe na kumpenda adui yake sababu alikuwa na Roho mtakatifu lakini ilikuwa ngumu kwa wafuasi wake kuelewa sababu walihishi kwa sheria na kufuata maongozi ya Daudi lakini wenyewe hawakujazwa Roho.Tofauti na sasa kila mtu amejaa Roho hivyo anawezeshwa kushinda vikwazo na kusamehe pia kuwapenda adui kutokana na nguvu ya Roho mtakatifu iliyo ndani yetu.(waefeso 3;20)Si vema katika vipengele vigumu kukwepa maagizo ya agano jipya na kukimbilia la kale ili kujifariji.Wengi wetu wanalipa kisasi na kujitetea kupitia maandiko na wengine wanalaani na kutoa maneno ya laana pengine hata madhabahuni na kutafuta maandiko ya kuwafariji.Biblia yapasa kuielewa kwa upana na kujifunza kwa umakini,si kila andiko utalitumia kwa wakati huu.mengine yaweza kusomwa kama historia au unabii uliopita,mengine ni ya sasa na yanahitaji kutekelezwa na mengine ni unabii ujao yapasa uyajue lakini usitumie kwa sasa kama utekelezaji utasababisha ajali katika uliwengu wa roho.Lakini yote tumewekewa ili tujifunze na tukiyaelewa yatatufaa.

Mtazamo wa sasa juu ya adui zetu ni;
(a)kupenda adui zetu(mathayo 5;44)
Upendo wetu tunarithishwa na Yesu.aliwapenda adui hata siku moja mbaya wake amebeba panga ili amkate Yesu,Petro akajibu mashambulizi kwa kumkata sikio,lakini Yesu akamponya sikio lake na akamruhusu aendelee na ubaya wake.(yohana 18:10 na luka22:50-51.)hili pendo ni la tofauti halifanani na halielezeki,Na ndilo analotuagiza Bwana wetu Yesu Kristo kuwapenda adui zetu kwa kiasi hicho hata wangepanga mabaya juu yako,wewe wapende,wakutengenezee kifo wewe wapende tu.maisha yako ni mali ya Mungu hakuna anaweza kuchukua kama umesimama kwa uaminifu kwa Mungu.
Mwenye kuhukumu ni Mungu tu na haki yako ipo mikononi mwake usitumie nguvu kujitetea kama petro,mwachie yeye mwenye kuhukumu.
Maisha ya Yesu ni kioo yapasa tuyaige.yeye hakupigana na adui kwa jinsi ya mwili nasi tufuate mfano wake.Pia Paulo anazidi kusisitiza kuwa vita yetu ni ya ulimwengu wa Roho(efeso 6:12)

(b)kubariki wanaotuudhi(warumi 12:14 na mathayo 5:44)
Tumeagizwa kubariki si kulaani,vinywa vyetu viponye.Watu wengine wanatumia mamlaka vibaya wengine utamka maneno ya laana katika madhabahu,hilo ni kosa kubwa.Yesu walimdhihaki wakamnena mabaya mpaka msalabani jibu alilosema"Baba uwasamehe hawajui watendalo",kipimo cha kujua kinywa cha mkristo kimejaza nini ni wakati wa jaribu.Wengine wanatoa matusi,maneno ya laana,lawama kuonyesha kuwa vinywa vimejaa uchafu.Bwana atakase kinywa chako wakati wote.maneno yako yawe heri na baraka kwa wengine.

(c)kuwatendea mema wanaotuchukia.
Yesu akasema akunyang'anyae kanzu mpe na joho(mathayo 5;40).Mtendee mema adui yako,akiumwa mpeleke hospital,akiwa na njaa mpe chakula.

(d)kuwaombea wanaotuudhi na kututesa.
Kama Yesu alivyowaombea nasi tuige mfano wake.Tusiwatakie mabaya lengo letu kubwa au ombi langu maadui zangu waokoke na wamjue Mungu ninayemwabudu simpangii Bwana waokoke lini lakini najua ipo siku wataokoka.Na Mungu ndiye aliyeumba mbaya na mwema na malipo ya mbaya anayo yeye,namwachia mwenye kuhukumu.Tusishindwe na ubaya wala tusiwe na kisasi(zab.34:13-14.)

TABIA NNE ZA  MATENDO YA BINADAMU
(a)mtu akikutendea mabaya na ukalipa mabaya huo ni ubinadamu(wanadamu wengi wanalipa baya kwa baya)
.(b)mtu akikutendea mema na ukalipa mabaya huo ni ushetani au uibilisi.(atendaye hayo anakuwa amerithi tabia ya shetani)malipo ya shetani hata ungemfurahisha kwa kumtumikia kwa nguvu mwisho wake ni kukuangamiza tu hawezi hata siku moja akakulipa mema kusudi lake tangu mwanzo ni kuua,kuchinja na kuharibu.Anaweza akakuvutia lakini hana nia njema ni kama mtu anayefuga kuku wa nyama.atawahudumia vizuri kuku,anawapa chakula,madawa wakiugua pengine kuku anaweza kuwaza huyu mtu ananipenda kumbe sivyo matokeo ya mwisho ya hao kuku ni kuchinjwa tu.usifanye urafiki na shetani kuna siku atakumaliza tu hata akufurahishe kuna siku atakuchinja.ACHANA NAYE KWA JINA LA YESU. 
(c)mtu akikutendea mabaya wewe ukalipa mema huo ni ukiUngu( au hiyo ndiyo tabia ya KIMUNGU. Na ndivyo biblia inaagiza juu ya adui zetu.atendaye hayo anapata thawabu kubwa kwa Mungu.Japo wanadamu wanaweza kukuona mjinga lakini mbele za Mungu una maana kwa tendo hilo. 
(d)ukitenda mema kwa mema huo ni ukiUngu au tabia apendayo Mungu japo ni tabia ambayo wanadamu wengi utenda pia(haiwezi kufanana na ile ya kulipa mema kwa aliyekutendea mabaya.kipimo cha mtu aliyeokoka kipo hapo na ni wachache wanaoshinda.

Mchungaji:Lugano Mwakisole
EAGT Paradise Mbagala Zakhem


Monday, August 11, 2014

BARAKA ZETU ZIPO KATIKA NENO.



Mchungaji Lugano Mwakisole

BARAKA  ZETU  ZIPO  KATIKA  NENO.
MATHAYO  4 :4  "mtu hataishi kwa mkate tu  bali  kwakila  neno litokalo  katika  kinywa  cha Mungu"
Wapendwa wasomaji napenda tushirikishane jambo kuu sana lina lohusu baraka.kila mtu anapenda baraka lakini ni muhimu kufahamu msingi wa baraka zetu tuliookoka unapatikana wapi,na wenzetu au mababa zetu wa Imani katika biblia walipata baraka kupitia nini?soma zaidi upate kuelewa.

KUNA TOFAUTI YA KUFANIKIWA NA KUBARIKIWA.
Mafanikio ni matokeo ya mwilini bali baraka zinaanza rohoni nakuonekana mwilini.Mtu aliyefanikiwa anaweza akawa na pesa,magari,majumba ya kifahari(matokeo ya nje) lakini akawa hana amani,furaha ya ki Mungu na upendo wa ki Mungu.pia ni mtu anayeishi kwa masharti mazito,na hofu tele juu ya utajiri wake,hii tena si baraka bali ni mafanikio tu,baraka ni matokeo ya rohoni kwanza inayobeba furaha,amani na upendo wa ki Mungu.Baraka inaanza rohoni kwa vitu hivyo nilivyovitaja(upendo,furaha na amani ya kiMungu) ndipo inadhihirika mwilini kama matokeo ya utajiri wa fedha,nyumba,magari nk.Mtu akipata vitu vya mwilini akakosa amani na vitu hivyo au furaha ya Mungu anakuwa ni mtu wa huzuni,anakosa upendo na ndugu zake au marafiki,mara nyingine anakuwa na ukali usio na sababu, msongo wa mawazo japo ana kila kitu.Anapungukiwa na baraka au vitu vya ndani (rohoni)vitakavyomfurahisha kwanza bali vinavyoonekana na matokeo yake yanakuwa ni mabaya.Anaweza kuacha vyote na ukashangaa analala kwa mganga wa kienyeji au mpunga pepo,katika mazingira machafu yasiyoendana na yeye.tatizo alidhani baraka zinaanzia mwilini kumbe baraka zinaanza rohoni na kumalizikia mwilini.maandiko yanasema"utafuteni kwanza ufalme wa Mungu na haki zake na mengine tutazidishiwa"Haki zinazosemwa hapo ndio hizo furaha amani pendo za kiMungu na mengine tunayozidishiwa ni utajiri tunaouona kama fedha, magari,majumba n.k Na baraka zetu zinajengwa na neno la Mungu na huu ndiyo msingi wetu.

 Maisha yetu,kuishi kwetu,kula  yetu,vaa  yetu  na  baraka  zetu  zimebebwa katika neno.  Na  hii  ndio  maana ya kusema tunaishi  kupitia  neno  analosema Mungu.(math 4:4).Pia  andiko  la EBRANIA 10 : 38 linasema "mwenye haki   wa mungu ataishi kwa imani" inapoongelewa imani  inamaanisha  kusikia neno la kristo ,(WARUMI 10 :17)  Hapo tunapata picha zaidi   kuwa maisha yetu  yote  na  mafanikio yamebebwa  na neno la Mungu:

Neno humjenga mtu katika imani  na  imani inasababisha  baraka zote za kimwili  na kiroho.watu wengi wanapenda kubarikwa lakini  hawataki kuishi kwa neno,kulisoma neno,au kusikia kupitia watumishi wa Mungu.Hawaendi kanisani kukutana na mtoa baraka kwa kisingizio wana kazi nyingi. Ni  vigumu watu  hawa kupata baraka za kiMungu.Baraka huja kupitia neno  la Mungu, unapolisikia na kulitendea  kazi ,  na Baraka inaanzia  rohoni  ndipo hudhihirika mwilini .Yohana aliandika waraka wake  " 3YOHANA 1 :2 mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na  Afya njema kama vile roho yako  ifanikiwavyo" akiwa anamanisha baraka zote zinaanza rohoni  ndipo inadhihirika mwilini

MIFANO YA WATU WALIOBARIKIWA KUPITIA NENO LA MUNGU
 1. Ibrahimu baba wa imani(MWANZO 12:1-3)
Ibrahimu aliambiwa neno na Mungu  atoke aende katika nchi  ambayo aliandaliwa baraka tele.
Baraka zilianza pale tu Ibrahimu alipotii neno au agizo na akatekeleza.mstari wa 4 ibrahim alitekeleza na alipotoka baraka zilimfuata kama neno liliivyomwambia.japo alipitia mitihani mingi lakini ushindi wa mwisho ulikuwa mkuu sana na matokeo yake ni makubwa,Tunaona matokeo ya taifa la israel ni kutokana na kutii kwa ibrahim.ishi kwa neno na kutii kama Ibrahim utaziona baraka kwako na familia yako na hata kizazi chako chote.   
2 NABII ELIYA:  WAFALME 17 :1-16
 Hapo tunaona maisha alioishi Eliya baada ya kutokea njaa iliyosababishwa na maombi yake mwenyewe. Baada ya kuzuia mvua kulikuwa na ukame   na njaa kubwa katika  mji wa israeli  wakati huo mgumu  watu wengi  walisumbuka  sana kutafuta chakula  lakini Eliya  kwake maisha hayakuwa magumu sababu  yeye aliishi kwa neno la Mungu.  
 Ukisoma mstari  2-7  Neno lilimjia Eliya  aende katika kijito cha kerithi. Alipotii  kwenda huko  Mungu alikuwa amemwandalia kunguru wamlishe  katika kijito  hicho na kunywa maji hayo.   wakati huo mgumu , Eliya haukumsumbua  kwasababu  yeye alitii neno la Bwana na aliweza kuishi.Hali ngumu za maisha  au kukosa pesa si sababu ya kukata tamaa kwani tukiamini neno lake,Mungu atafungua njia juu yetu.kumbuka neno linasema "dunia na vyote viijazavyo ni mali ya Bwana,ZABURI 24:1.Pia anatupa ahadi kuwa tukimwomba yeye atatupa kwa kuwa na sisi ni watoto wake.(MATH 7:7-11)
Mstari 8:16  katika 1wafalme 17 tumeona kijito  kilikauka kutokana  na hali ya ukame, lakini  hilo  halikumtisha  Eliya  bali alisikiliza maelekezo ya neno.  Ndipo neno likamwongoza kwenda kwa mwanamke mjane wa serepta na akafanya muujiza kupitia mafuta kidogo  katika chupa na unga kidogo. Na muujiza mkubwa ukafanyika wakaishi.
   Eliya hakutishwa na mabadiliko ya hali ya hewa bali aliamini neno kuwa litamfanya aishi . Je  ni kitu gani kinakufanya uwe na hofu ya maisha, je kukosa kazi, mabadiliko ya uchumi, au kukataliwa na ndugu au jamaa.? Vyote hivyo haviwezi  kuzuia baraka zetu sababu sisi hatuishi kwa bahati(hatubahatishi  maisha)  bali maisha yetu yanaongozwa na neno (MATHAYO 4:4).Watu wasiookoka wanaishi kwa bahati na ndio maana wanaishi kwa wasiwasi na wengine husema "bahati hairudi mara mbili"sababu wanabahatisha wanakuwa na hofu wakifilisika utakuwa ndio mwisho wao.Sisi tuliookoka tunaishi kwa neno au maongozi ya neno na baraka zetu ni nyingi hata zikizuiliwa na shetani au watu wenye hila sehemu fulani,iwe kufukuzwa kazi,kudhurumiwa,kutendewa mabaya na  watu  tuliowaamini lakini wakageuka,bado Mungu atafungua kwa njia nyingine. Sisi ni wabarikiwa na ni kipawa tulichopewa kama biblia isemavyo"kipawa ni kito cha thamani na kila kigeukapo hufanikiwa,)Maana ya kila kigeukapo inamaanisha kila uendapo na kila ufanyacho utafanikiwa.Shetani japo alijaribu kugusa maisha ya Ayubu kwa magonjwa,kuuwa watoto wake na mifugo na mali zake kufilisiiwa,bado alimtegemea Mungu na matokeo ya mwisho yalikuwa mazuri kuliko mwanzo na alipata utajiri mwingi kuliko mwanzo.Hata kama shetani alichezea uchumi wako na ukakata tamaa,nakutia moyo kuwa baraka yako bado ipo si za kubahatisha,Yesu atakubariki kwani anazo baraka nyingi.Pia baraka zetu zinatufuata popote tunapoenda kama neno lisemavyo " hakika wema na fadhiri  zitatufuata  siku zote za maisha yetu, ZABUR 23:6"
Pia baraka zetu anayetoa ni Mungu na ndie anatupa nguvu za kupata utajiri(  KUMB 8:17:18)  Wala si uwezo wetu hivyo tumtegemee yeye  ambae ndiye neno  (YOHAN 1:1)  Ili atupe mahitaji yetu,

 Vitu vyote vipo chini yake na anatoa kwakila mtu anaye mcha na kumtii( 1MAMB NYKT 29:12).

Ushauri wangu kwako mpe Yesu maisha yako utapata baraka za Bwana ambazo zinajumuishwa na upendo,furaha,na amani kisha utajiri wa fedha,mifugo,mashamba,majumba,magari n.k Bwana atatuzidishia na baraka ya Mungu inaenda hatua kwa hatua,yapasa uwe mvumilivu kama baba yetu Ibrahim aliyepita wakati mgumu lakini mwisho wake ulikuwa mzuri.Usitake utajiri kwa haraka dunia itakupoteza.wengi tunawaona walitaka utajiri kwa haraka lakini wamekufa mapema tena kwa vifo vya kuhuzunisha na pesa na utajiri wao hawakuufaidi bali wamefaidika wengine.Baraka ya Mungu hutajirisha na haichangamani na majuto.Mungu awabariki.

Kwa Msaada Zaidi
Waweza kuwasiliana nami
0688387834
luggymakky@gmail.com

Monday, August 4, 2014

Karibuni kwenye maombi ya jioni kanisani Eagt Paradise Church yanaanza saa 12:00 jioni mpaka saa 2:00 usiku

Karibuni kwenye maombi ya jioni kanisani Eagt Paradise Church yanaanza saa 12:00 jioni mpaka saa 2:00 usiku

by Eagt Paradise



August 04, 2014 at 04:25PM

from Facebook

via IFTTTfrom Facebook

via IFTTT