EAGT PARADISE ni kanisa la Kipentekoste lililo chini ya EAGT, Kanisa hili lipo Mbagala Zakhem,karibu na viwanja vya wazi Zakhem(Kwa watengeneza masofa), PARADISE linaongozwa na Mtumishi wa Mungu Mchungaji Lugano Mwakisole.
Friday, September 5, 2014
Thursday, September 4, 2014
KUWA RAFIKI WA KARIBU WA YESU-Somo linaendelea:Mch Lugano Mwakisole
| MCHUNGAJI LUGANO MWAKISOLE |
KUWA RAFIKI WA KARIBU WA YESU
Mungu ni mwema ametukutanisha tena katika Blog hii ili kujifunza neno lake,
Leo tutaendelea kujifunza HATUA ZA KUWA RAFIKI WA KARIBU WA YESU,
Juma liliopita tulijifunza hatua nne na leo tutaendelea na hatuna nyingine,
Kama hukusoma hatua ya kwanza mpaka ya tatu bofya hapa
HATUA ZA KUWA RAFIKI WA KARIBU WA YESU
4.Hatua ya nne ni kushiriki mateso pamoja naye(1Petro4:12-16)
-Unapokuwa rafiki wa Yesu hautapata raha tu bali na mateso pia.Yesu anaruhusu mateso na majaribu yakupate ili kupima urafiki wenu upo imara au la.Kila mtu aliitwa na Yesu na kuokoka kwa njia tofauti.Wengine waliitwa kwa kuponywa magonjwa mbalimbali,wengine waliombewa wakapata ajira au kupandishwa vyeo makazini ndipo walipoamua kuokoka,wengine walipoombewa biashara zao zikafanikiwa wakachukua uamuzi wa kuokoka.Vyote hivi vilikuwa vivutio vya wokovu kwa upande mmoja,Na kila mtu alipopata baraka hizi alishuuhudia kwa ujasiri na aliuona upendo wa Yesu ulivyo mkuu na wa ajabu.Lakini kuna kiwango kingine cha kuuona upendo wa Yesu katika majaribu,dhiki,udhia,msiba,magonjwa,kukosa kazi,kukosa hata familia kwa ajili ya Yesu. Hapa anatafutwa mwanafunzi kwelikweli au rafiki wa Yesu atakayeshinda mapito yote na kustahimili.
Ona Mifano hii:-
1-Wanafunzi wawili walimwomba Yesu mmoja akae kulia kwake na mwingine kushoto katika ufalme wake.(Mathayo 20:20)Yesu aliwauliza nao kama kweli wataweza kukinywea kikombe chake? akimaanisha wanaweza kushiriki mateso pamoja naye? Kutaka kuwa karibu naye ni kukubali kushiriki mateso naye.Ni wengi hupenda kuwa karibu naye lakini hawawezi kushiriki Mateso pamoja naye.Baada ya muda kupita Yesu aliwachukua wale wanafunzi ili kuwapima kama kweli wanaweza kukinywea kikombe pamoja naye lakini wakati wa kuomba wanamwacha Yesu peke yake,wanalala.(Math 26:37).Ili uwe rafiki wa karibu wa Yesu ni lazima ukubali kushiriki mateso naye.
2-kuna sehemu nyingine naipenda wakati Yesu amegawa mikate kulisha makutano,walikula watu elfu tano hao ni wanaume tu,ukichanganya na wanawake na watoto ni umati mkubwa sana wa watu pengine ingekuwa vigumu hata kuhesabu.(Yohana6:1-11),lakini siku zilipofuata Yesu anabadilisha chakula kawaambia wale mwili wake na wanywe damu yake,(Yohana 6:26-58) hapa watu wote wakakimbia walibaki waume kumi na mbili tu.Lilikuwa fumbo zito akimaanisha kwake hakuna mikate tu yaani miujiza tu au raha tu kuna kushiriki mwili na damu ikimaanisha kushiriki mateso pamoja naye,na hapa yanamaanisha mateso ya msalaba(Mathayo 26:28).Msalaba ni kukubali kuteseka kwa ajili ya Yesu,kukubali hata kukosa mume au mke au kufukuzwa na wazazi sababu ya kuokoka.(Mathayo 10:34-39)msalaba ni kujikana na kumfuata Yesu inabidi ujitoe kwa dhati.Kubali hata kupoteza utu wako,familia,mume au mke kwa ajili ya Yesu.
-pia ni lazima ukubali kujikana na kubeba msalaba(Mathayo16:24-27).msalaba ni mateso lakini ndiyo ushindi wetu,msalaba ni aibu,kubali aibu kwa ajili ya Kristo.Kubali kunenwa kuwa umechanganyikiwa,kuacha starehe,anasa,dhambi zote hata kama zinavutia kwa ajili ya kristo.unaweza ukaona wenzako kazini wanaiba kwa kuchengesha mahesabu na unaona wanafanikiwa kuwa na nyumba nzuri,magari n.k.wewe usifuatishe acha,jikane,huko ndiko kubeba msalaba.
-Naomba nikukumbushe tenzi za Rohoni wimbo usemao" Bwana u sehemu yangu "kuna mahali mtunzi ameandika"mahali hapa sikutaka niheshimiwe na yanikute mateso sawa sawa na wewe."na chorus yake inasema pamoja na wewe ukimaanisha ushirika na Yesu katika mateso pia.ILI UWE RAFIKI WA YESU KUBALI KUSHIRIKI MATESO PAMOJA NAYE.
5.Hatua ya tano ni uaminifu.(1Kor 4:1-2),Rafiki wa Yesu anajua siri za Mungu nyingi anatakiwa kuwa mwaminifu sana,neno hili kuna maneno mawili ambayo imani na kamili.ili mtu awe mwaminifu lazima awe na imani kamili au imani iliyojitosheleza(faithfull).Na imani kamili ndiyo inatimizwa na kutii kila amri ya kwenye biblia.Kuna siri nyingi utapewa kama rafiki yake na si zote za kusema kwa wakati huo,nyingine unaweza kuambiwa uombe wewe mwenyewe,na nyingine utekeleze kwa matendo,nyingine anaweza kukwambia kama rafiki yake mpendwa lakini hazina utekelezaji japo kakushirikisha,zipo katika mapenzi yake hauwezi badilisha.(Zaburi25:14)
Mfano:
Mungu anaweza kukuambia habari ya mtu kuwa atamchukua au kifo kitampata.hapo pana mambo ya kuzingatia.Je Mungu ameruhusu au ni roho ya mauti.kama roho ya mauti unaweza kukemea lakini kama ni mapenzi yake unapaswa kushukuru.lakini pia inaweza ikawa mapenzi yake lakini ukamsihi asimchukue kwa kupeleka hoja zenye nguvu kwake na kumsihi kama ombi lakini si amri.Yesu aliomba baba ikiwezekana kikombe kiniepuke.sehemu hiyo akutumia mamlaka sababu ni sehemu ambayo ilikuwa katika mamlaka ya Mungu.ni lazima uelewe maombi ya kusihi mapenzi ya Mungu na sehemu ya kutumia mamlaka.Sisi tumepewa kumtii Kristo pia tumepewa kumpinga shetani(Yakobo 4:7)Tukiomba vibaya bila kuelewa hatupati majibu.Mtu anayefikia hatua ya kuwa mwaminifu ataambiwa siri na Mungu hata za mambo yanayotokea mbele kama misiba,baraka,njaa,vita n,k,mengine ni ya kusema na mengine si ya kusema inategemea na maongozi ya Roho Mtakatifu.Mtu mropokaji sana ,asiyetulia,hawezi kupewa siri nyingi.anatafutwa MWAMINIFU ndiye anastahili kuambiwa mambo ya Bwana na atasema kwa maongozi ya Roho tu.Utulivu wa Yohana ulimsaidia kuandika kitabu cha ufunuo chenye siri kubwa juu ya siku za mwisho.Mungu alimteua Musa kuongea naye na kisha kupeleka maagizo kwa Israel.Musa alijua siri za Mungu kutokana na uaminifu wake.maono mengine Mungu anaweza kukupa lakini si ya sasa,ukikurupuka kusema yanaweza kukuletea matatizo.Manabii walipewa mambo ya miaka mingi ijayo na mpaka wanakufa hawakuyaona.wengine wakiambiwa upenda kusema haraka ili wajikweze kuwa wenyewe ni manabii wa kweli.Watu kama hao ni rahisi kushuswa au kutopewa tena.
Mungu awabariki somo litaendelea ili kuzifahamu faida za kuwa rafiki wa Yesu.
Video ya somo hili:https://www.youtube.com/watch?v=qoBJ4EJZmMU
Mchungaji:Lugano Mwakisole
EAGT Paradise Mbagala Zakhem
Monday, September 1, 2014
Sunday, August 31, 2014
Wednesday, August 27, 2014
KUWA RAFIKI WA KARIBU WA YESU-Mch.Lugano Mwakisole
| MCHUNGAJI LUGANO MWAKISOLE |
KUWA RAFIKI WA KARIBU WA YESU
Kuna utofauti mkubwa kuwa
rafiki na mwanafunzi,
Kuwa rafiki wa Yesu ni zaidi
ya kuwa mwanafunzi wake,Ni kiwango ambacho si rahisi kwa mwamini kufikia kuwa
rafiki wa Karibu wa Yesu,Ni hatua ya juu sana
Ukiwa rafiki wa Yesu unapata
nafasi ya kuongaea na nae ana kwa ana,
Katika Somo hili tutajifunza
Jinsi Gani sisi kama wanafunzi wa Yesu tunaweza kuwa Rafiki zake wa
karibu.Fuata nami na Mungu atakubariki
HATUA ZA KUWA RAFIKI WA YESU.
1.UTII
hatua hii ni ya muhimu sana
ili ufikie kuwa rafiki.Yesu amesema ninyi mmekuwa rafiki zangu mkitenda
niwaamuruyo(Yohana 15:14),Yesu anathibitisha kuwa ili tuwe marafiki zake ni
lazima tutii maagizo yake..kipimo cha kumpenda Yesu ni kutii maagizo
yake.pia katika Yohana 14:21 inasema "Yeye aliye na amri zangu, na
kuzishika,yeye ndiye anipendaye;naye anipendaye atapendwa na Baba yangu,nami
nitampenda na kujidhihirisha kwake" mtu anayeshika amri au maagizo ya Yesu
ndiye ependwaye na Yesu au anakuwa rafiki wa Yesu.Yesu alimuuliza Petro mara
tatu kama kweli anampenda.(Yohana 21:15-17),Petro alipojitetea kwa sababu
nyingi na kutaka kuonyesha kuwa anampenda Yesu alimjibu kuwa achunge na kulisha
kundi.Kumbuka alimuuliza maswali haya baada ya kufufuka akisikitishwa na Petro
kuacha kutii wito aliomwachia kabla ya kufa na malezi yote aliyompa kwa
muda wote aliokaa naye.pia alipomwita aliwambia aache kuvua samaki naye
atamfanya kuwa mvuvi wa watu.Muda mfupi tu Yesu alipomwacha ameacha kutii agizo
ameenda kuvua samaki.kitendo cha kutokutii wito Yesu akahuzunika sana na
kumuuliza kweli anampenda? Tatizo ni kutokutii ndicho Yesu kilichomsononesha.Pia
lazima tujiulize mbona anaulizwa Petro si wanafunzi wengine?wakati kwenye kuvua
samaki walikuwa wengi,Jibu ni hili Yesu hakutegemea rafiki yake mpendwa au mwanafunzi
wa karibu zaidi ndio kaharibu.Ukiwa rafiki wa Yesu ni lazima uwe na utii wa hali
ya juu katika maagizo ndipo Yesu atakuwa na imani nawe.usifanye kitu
kitakachosababisha Yesu kuwa na mashaka na urafiki wenu kama Petro.Mimi na wewe
tujiulize je tumesimamia wito wetu na kutii kila agizo ili Yesu atupende
kama rafiki zake?
2.KUPENDA KUJIFUNZA
Hii ni hatua ya muhimu na
Yesu anaizingatia sana kwa marafiki zake.(Yohana 8:31) Yesu anasema “ninyi
mkishika neno langu mmekuwa wanafunzi wangu kwelikweli” kuwa mwanafunzi
kwelikweli kwa maana nyingine ni kuwa mwanafunzi anayepita wanafunzi wengine au
kuwa rafiki wa karibu.Tuna mfano wa dada aliyekuwa rafiki sana wa Yesu anaitwa
Mariam.alikaa miguuni pa Yesu akijifunza.(luka 10:38-42) Yesu alimpenda na
akasema amechagua fungu jema,na kihistoria anaonyesha ni miongoni mwa rafiki wa
karibu wa Yesu.Sehemu nyingi zinaonyesha kama kufa kwake,kufufuka kwake,na mpaka
anapaa alikuwa karibu naye sana.
3.HATUA YA UTOAJI
Hii ni sadaka ya tofauti na sadaka
ya kawaida.sadaka ambayo inamgusa Yesu kwa kiwango cha juu.Sadaka ambayo Yesu
akiangalia inamkumbusha sadaka yake kubwa aliyoitoa msalabani.ukitoa sadaka ya
namna hiyo ni lazima Yesu awe rafiki yako.sadaka hiyo inakufanya wewe
uchukuliwe uwe karibu na sadaka ya msalaba.Watu wengi waliotoa kwa kiwango cha
juu kama hicho waliugusa moyo wa Yesu na kuwa marafiki zake.
-Mfano wa kwanza ni baba wa
imani Ibrahim alikubali kumtoa mwanawe wa pekee Isaka kuwa sadaka ya
kuteketezwa.kitendo cha kutoa mtoto wa pekee ,mpendwa,kilimkumbusha Mungu
kumtoa mwanawe wa pekee Yesu kufa msalabani. Unaweza kusema mbona wakati huo
Yesu alikuwa bado hajafa.kumbuka mpango wa Yesu kufa ulipangwa na Mungu zamani
sana biblia inasema kabla ya kuwekwa misingi ya dunia(1petro1:19-20) kwahiyo
utoaji wa Ibrahim ulikuwa utabiri wa Yesu na ulimfanya Ibrahim kumkumbusha
Mungu sadaka yake.habari yote unaipata katika kitabu cha mwanzo 22.sura
yote.Pia tunaona katika msitari wa 11-12 malaika wa Bwana anamsifia Ibrahim kwa
moyo wake wa kumcha Bwana.Mungu aliuona moyo wa Ibrahim baada ya kutoa sadaka
ya tofauti.urafiki wa MUNGU na Ibrahim uliongezeka.
Mstari wa 13 Mungu
anatoa kondoo badala ya Isaka,hapa inafundisha kuwa yeyote atakayetoa kwa kiwango
cha juu na sadaka ya pekee,maalumu au inayogusa moyo wake Mungu lazima atoe
mbadala kwa lugha nyingine Mungu atakulipa kwa njia tofauti kama Ibrahim
alivyolipwa
(mst 15-18)
-Mfano mwingine ni Mariam Magdalena.pamoja
na kukaa miguuni pa Yesu na kujifunza lakini pia alimtegemeza Yesu kwa mali
zake.kuna sadaka moja ilimgusa Yesu,alipompaka Yesu kwa mafuta ya
thamani.katika desturi ya wayahud kulikuwa na kutawadha miguu na hii ilikuwa kwa
mtumwa kutawadha Bwana wake.Mariam hakutumia kitambaa,yeye akatumia
nywele za kichwa chake,pia wengine walitumia maji lakini yeye alitumia machozi
yake na mafuta ya thamani.(Yohana 12:3 na luka7:36-38)kitendo hiki kiligusa
moyo wa Yesu na kilimshangaza,mafuta thamani kubwa kumtawadha Yesu,ni sadaka kubwa
sana alitoa.Unyenyekevu wa Mariam(kudondosha machozi ishara ya maombi na
kumfuta kwa nywele zake kuonyesha kushuka),sadaka yake kubwa(kitendo cha
kutojari mali zake kwaajili ya Yesu)na kupenda kukaa miguuni pa Yesu na
kujifunza kilifanya Yesu awe rafiki yake zaidi ya wanafunzi wengine.
Bado kuna hatua nyingine tatu
ili kukamilisha kuwa rafiki wa Yesu,tutaendelea nazo wiki ijayo siku kama
hii.Ombi langu tafuta kuwa rafiki wa Yesu utapata faida nyingi ambazo
utazifahamu utakapoendelea na somo mpaka mwisho.
MUNGU AWABARIKI.
Mchungaji:Lugano Mwakisole
EAGT Paradise Mbagala Zakhem
Tuesday, August 26, 2014
Monday, August 25, 2014
IBADA YA JUMAPILI 24.8.2014 KATIKA PICHA
| Mtumishi wa Mungu Majaliwa akimtukuza Mungu kwa wimbio wake "KWA MSAADA WA ROHO" |
| Mama Mchungaji akimtumikia Mungu kwa njia ya Uimbaji |
| Kwaya ya Kanisa ikihudumu |
| Kwaya ya Kanisa ikihudumu |
| Kwaya ya Kanisa ikihudumu |
| Kwaya ya Kanisa ikihudumu |
| Kwaya ya Kanisa ikihudumu |
| Mzee wa Kanisa Shedrack |
| Mtumishi wa Mungu,Mch.Lugano Mwakisole akileta kusudi la Mungu kwa Kusanyiko |
| Wakati wa Maombezi |
Wednesday, August 20, 2014
Tuesday, August 19, 2014
AGANO JIPYA JUU YA ADUI ZETU-Mch.Lugano Mwakisole
MCHUNGAJI LUGANO MWAKISOLE
AGANO JIPYA JUU YA ADUI ZETU.
(Math.5:43-47)
Leo
ninapenda tushirikishane mtazamo wa agano jipya juu ya adui zetu.
Mtazamo wa
agano la kale na agano jipya ni tofauti.Agano la kale(torati)kwa sehemu
linasema jino kwa jino au linaruhusu kulipa baya kwa baya lakini ni
tofauti na agano jipya linaagiza kuwatendea mema adui zetu.Si kwamba biblia
inapingana,kila watu walipewa maagizo na namna ya kuishi kwa wakati wake.sisi
tupo kipindi cha agano jipya na maagizo ya Yesu aliyoyatoa ni tofauti na ya
kale.
Maagizo tuliyopewa ni magumu zaidi na hii inatokana na pia tuna uwezo
mkubwa wa kushinda sababu tuna neema zaidi kutokana na ukombozi wa Yesu pia
tuna Roho Mtakatifu aliyemwagwa kwa wote tofauti na zamani ilikuwa kwa watu
maalumu.Daudi aliweza kusamehe na kumpenda adui yake sababu alikuwa na Roho
mtakatifu lakini ilikuwa ngumu kwa wafuasi wake kuelewa sababu walihishi kwa
sheria na kufuata maongozi ya Daudi lakini wenyewe hawakujazwa Roho.Tofauti na
sasa kila mtu amejaa Roho hivyo anawezeshwa kushinda vikwazo na kusamehe pia
kuwapenda adui kutokana na nguvu ya Roho mtakatifu iliyo ndani yetu.(waefeso
3;20)Si vema katika vipengele vigumu kukwepa maagizo ya agano jipya na kukimbilia
la kale ili kujifariji.Wengi wetu wanalipa kisasi na kujitetea kupitia maandiko
na wengine wanalaani na kutoa maneno ya laana pengine hata madhabahuni na
kutafuta maandiko ya kuwafariji.Biblia yapasa kuielewa kwa upana na kujifunza
kwa umakini,si kila andiko utalitumia kwa wakati huu.mengine yaweza kusomwa
kama historia au unabii uliopita,mengine ni ya sasa na yanahitaji kutekelezwa
na mengine ni unabii ujao yapasa uyajue lakini usitumie kwa sasa kama
utekelezaji utasababisha ajali katika uliwengu wa roho.Lakini yote tumewekewa
ili tujifunze na tukiyaelewa yatatufaa.
Mtazamo wa sasa juu ya adui zetu ni;
(a)kupenda adui zetu(mathayo 5;44)
Upendo wetu tunarithishwa na Yesu.aliwapenda adui hata siku
moja mbaya wake amebeba panga ili amkate Yesu,Petro akajibu mashambulizi kwa
kumkata sikio,lakini Yesu akamponya sikio lake na akamruhusu aendelee na ubaya
wake.(yohana 18:10 na luka22:50-51.)hili pendo ni la tofauti halifanani na
halielezeki,Na ndilo analotuagiza Bwana wetu Yesu Kristo kuwapenda adui zetu kwa kiasi hicho hata
wangepanga mabaya juu yako,wewe wapende,wakutengenezee kifo wewe wapende
tu.maisha yako ni mali ya Mungu hakuna anaweza kuchukua kama umesimama kwa
uaminifu kwa Mungu.
Mwenye kuhukumu ni Mungu tu na haki yako ipo mikononi mwake
usitumie nguvu kujitetea kama petro,mwachie yeye mwenye kuhukumu.
Maisha ya Yesu
ni kioo yapasa tuyaige.yeye hakupigana na adui kwa jinsi ya mwili nasi tufuate
mfano wake.Pia Paulo anazidi kusisitiza kuwa vita yetu ni ya ulimwengu wa
Roho(efeso 6:12)
(b)kubariki wanaotuudhi(warumi 12:14 na mathayo 5:44)
Tumeagizwa kubariki si kulaani,vinywa vyetu viponye.Watu wengine wanatumia mamlaka vibaya wengine utamka maneno ya laana katika madhabahu,hilo
ni kosa kubwa.Yesu walimdhihaki wakamnena mabaya mpaka msalabani jibu
alilosema"Baba uwasamehe hawajui watendalo",kipimo cha kujua kinywa cha
mkristo kimejaza nini ni wakati wa jaribu.Wengine wanatoa matusi,maneno ya
laana,lawama kuonyesha kuwa vinywa vimejaa uchafu.Bwana atakase kinywa chako
wakati wote.maneno yako yawe heri na baraka kwa wengine.
(c)kuwatendea mema wanaotuchukia.
Yesu akasema akunyang'anyae kanzu mpe na joho(mathayo
5;40).Mtendee mema adui yako,akiumwa mpeleke hospital,akiwa na njaa mpe chakula.
(d)kuwaombea wanaotuudhi na kututesa.
Kama Yesu alivyowaombea nasi tuige mfano wake.Tusiwatakie
mabaya lengo letu kubwa au ombi langu maadui zangu waokoke na wamjue Mungu
ninayemwabudu simpangii Bwana waokoke lini lakini najua ipo siku wataokoka.Na
Mungu ndiye aliyeumba mbaya na mwema na malipo ya
mbaya anayo yeye,namwachia mwenye kuhukumu.Tusishindwe na ubaya wala tusiwe na
kisasi(zab.34:13-14.)
TABIA NNE ZA MATENDO YA BINADAMU
(a)mtu akikutendea mabaya na ukalipa mabaya huo ni
ubinadamu(wanadamu wengi wanalipa baya kwa baya)
.(b)mtu akikutendea mema na ukalipa mabaya huo ni ushetani
au uibilisi.(atendaye hayo anakuwa amerithi tabia ya shetani)malipo ya shetani
hata ungemfurahisha kwa kumtumikia kwa nguvu mwisho wake ni kukuangamiza
tu hawezi hata siku moja akakulipa mema kusudi lake tangu mwanzo ni
kuua,kuchinja na kuharibu.Anaweza akakuvutia lakini hana nia njema ni kama mtu
anayefuga kuku wa nyama.atawahudumia vizuri kuku,anawapa chakula,madawa
wakiugua pengine kuku anaweza kuwaza huyu mtu ananipenda kumbe sivyo matokeo ya
mwisho ya hao kuku ni kuchinjwa tu.usifanye urafiki na shetani kuna siku
atakumaliza tu hata akufurahishe kuna siku atakuchinja.ACHANA NAYE KWA JINA LA
YESU.
(c)mtu akikutendea mabaya wewe ukalipa mema huo ni ukiUngu(
au hiyo ndiyo tabia ya KIMUNGU. Na ndivyo biblia inaagiza juu ya adui
zetu.atendaye hayo anapata thawabu kubwa kwa Mungu.Japo wanadamu wanaweza
kukuona mjinga lakini mbele za Mungu una maana kwa tendo hilo.
(d)ukitenda mema kwa mema huo ni ukiUngu au tabia apendayo
Mungu japo ni tabia ambayo wanadamu wengi utenda pia(haiwezi kufanana na ile ya
kulipa mema kwa aliyekutendea mabaya.kipimo cha mtu aliyeokoka kipo hapo na ni
wachache wanaoshinda.
Mchungaji:Lugano Mwakisole
EAGT Paradise Mbagala Zakhem
Monday, August 11, 2014
BARAKA ZETU ZIPO KATIKA NENO.
MATHAYO 4 :4 "mtu hataishi kwa mkate tu
bali kwakila neno litokalo katika kinywa
cha Mungu"
Wapendwa wasomaji napenda tushirikishane jambo kuu sana lina
lohusu baraka.kila mtu anapenda baraka lakini ni muhimu kufahamu msingi wa
baraka zetu tuliookoka unapatikana wapi,na wenzetu au mababa zetu wa Imani katika biblia
walipata baraka kupitia nini?soma zaidi upate kuelewa.
KUNA TOFAUTI YA KUFANIKIWA NA KUBARIKIWA.
Mafanikio ni matokeo ya mwilini bali baraka zinaanza rohoni
nakuonekana mwilini.Mtu aliyefanikiwa anaweza akawa na pesa,magari,majumba ya
kifahari(matokeo ya nje) lakini akawa hana amani,furaha ya ki Mungu na upendo wa
ki Mungu.pia ni mtu anayeishi kwa masharti mazito,na hofu tele juu ya utajiri
wake,hii tena si baraka bali ni mafanikio tu,baraka ni matokeo ya rohoni kwanza
inayobeba furaha,amani na upendo wa ki Mungu.Baraka inaanza rohoni kwa vitu
hivyo nilivyovitaja(upendo,furaha na amani ya kiMungu) ndipo inadhihirika
mwilini kama matokeo ya utajiri wa fedha,nyumba,magari nk.Mtu akipata vitu vya
mwilini akakosa amani na vitu hivyo au furaha ya Mungu anakuwa ni mtu wa
huzuni,anakosa upendo na ndugu zake au marafiki,mara nyingine anakuwa na ukali
usio na sababu, msongo wa mawazo japo ana kila kitu.Anapungukiwa na baraka au
vitu vya ndani (rohoni)vitakavyomfurahisha kwanza bali vinavyoonekana na
matokeo yake yanakuwa ni mabaya.Anaweza kuacha vyote na ukashangaa analala kwa
mganga wa kienyeji au mpunga pepo,katika mazingira machafu yasiyoendana na
yeye.tatizo alidhani baraka zinaanzia mwilini kumbe baraka zinaanza rohoni na
kumalizikia mwilini.maandiko yanasema"utafuteni kwanza ufalme wa Mungu na
haki zake na mengine tutazidishiwa"Haki zinazosemwa hapo ndio hizo furaha
amani pendo za kiMungu na mengine tunayozidishiwa ni utajiri tunaouona kama
fedha, magari,majumba n.k Na baraka zetu zinajengwa na neno la Mungu na huu
ndiyo msingi wetu.
Maisha yetu,kuishi kwetu,kula yetu,vaa
yetu na baraka zetu zimebebwa katika neno.
Na hii ndio maana ya kusema tunaishi kupitia
neno analosema Mungu.(math 4:4).Pia andiko la EBRANIA
10 : 38 linasema "mwenye haki wa mungu ataishi kwa imani"
inapoongelewa imani inamaanisha kusikia neno la kristo ,(WARUMI 10
:17) Hapo tunapata picha zaidi kuwa maisha yetu yote
na mafanikio yamebebwa na neno la Mungu:
Neno humjenga mtu katika imani na imani
inasababisha baraka zote za kimwili na kiroho.watu wengi wanapenda
kubarikwa lakini hawataki kuishi kwa neno,kulisoma neno,au kusikia
kupitia watumishi wa Mungu.Hawaendi kanisani kukutana na mtoa baraka kwa
kisingizio wana kazi nyingi. Ni vigumu watu hawa kupata baraka za
kiMungu.Baraka huja kupitia neno la Mungu, unapolisikia na kulitendea
kazi , na Baraka inaanzia rohoni ndipo hudhihirika
mwilini .Yohana aliandika waraka wake " 3YOHANA 1 :2 mpenzi naomba
ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na Afya njema kama vile roho yako
ifanikiwavyo" akiwa anamanisha baraka zote zinaanza rohoni
ndipo inadhihirika mwilini
MIFANO YA WATU WALIOBARIKIWA KUPITIA NENO LA MUNGU.
1. Ibrahimu baba wa imani(MWANZO 12:1-3)
Ibrahimu aliambiwa neno na Mungu atoke aende katika
nchi ambayo aliandaliwa baraka tele.
Baraka zilianza pale tu Ibrahimu alipotii neno au agizo na
akatekeleza.mstari wa 4 ibrahim alitekeleza na alipotoka baraka zilimfuata kama
neno liliivyomwambia.japo alipitia mitihani mingi lakini ushindi wa mwisho
ulikuwa mkuu sana na matokeo yake ni makubwa,Tunaona matokeo ya taifa la israel
ni kutokana na kutii kwa ibrahim.ishi kwa neno na kutii kama Ibrahim utaziona
baraka kwako na familia yako na hata kizazi chako chote.
2 NABII ELIYA: WAFALME 17 :1-16
Hapo tunaona maisha alioishi Eliya baada ya kutokea njaa iliyosababishwa na maombi yake mwenyewe. Baada ya kuzuia mvua kulikuwa na ukame na njaa kubwa katika mji wa israeli wakati huo mgumu watu wengi walisumbuka sana kutafuta chakula lakini Eliya kwake maisha hayakuwa magumu sababu yeye aliishi kwa neno la Mungu.
Hapo tunaona maisha alioishi Eliya baada ya kutokea njaa iliyosababishwa na maombi yake mwenyewe. Baada ya kuzuia mvua kulikuwa na ukame na njaa kubwa katika mji wa israeli wakati huo mgumu watu wengi walisumbuka sana kutafuta chakula lakini Eliya kwake maisha hayakuwa magumu sababu yeye aliishi kwa neno la Mungu.
Ukisoma mstari 2-7 Neno lilimjia Eliya
aende katika kijito cha kerithi. Alipotii kwenda huko Mungu
alikuwa amemwandalia kunguru wamlishe katika kijito hicho na kunywa
maji hayo. wakati huo mgumu , Eliya haukumsumbua kwasababu
yeye alitii neno la Bwana na aliweza kuishi.Hali ngumu za maisha au
kukosa pesa si sababu ya kukata tamaa kwani tukiamini neno lake,Mungu atafungua
njia juu yetu.kumbuka neno linasema "dunia na vyote viijazavyo ni mali ya
Bwana,ZABURI 24:1.Pia anatupa ahadi kuwa tukimwomba yeye atatupa kwa kuwa na
sisi ni watoto wake.(MATH 7:7-11)
Mstari 8:16 katika 1wafalme 17 tumeona kijito
kilikauka kutokana na hali ya ukame, lakini hilo
halikumtisha Eliya bali alisikiliza maelekezo ya neno.
Ndipo neno likamwongoza kwenda kwa mwanamke mjane wa serepta na akafanya
muujiza kupitia mafuta kidogo katika chupa na unga kidogo. Na muujiza
mkubwa ukafanyika wakaishi.
Eliya hakutishwa na mabadiliko ya hali ya hewa
bali aliamini neno kuwa litamfanya aishi . Je ni kitu gani kinakufanya
uwe na hofu ya maisha, je kukosa kazi, mabadiliko ya uchumi, au kukataliwa na
ndugu au jamaa.? Vyote hivyo haviwezi kuzuia baraka zetu sababu sisi hatuishi
kwa bahati(hatubahatishi maisha) bali maisha yetu yanaongozwa na
neno (MATHAYO 4:4).Watu wasiookoka wanaishi kwa bahati na ndio maana wanaishi
kwa wasiwasi na wengine husema "bahati hairudi mara mbili"sababu
wanabahatisha wanakuwa na hofu wakifilisika utakuwa ndio mwisho wao.Sisi
tuliookoka tunaishi kwa neno au maongozi ya neno na baraka zetu ni nyingi hata
zikizuiliwa na shetani au watu wenye hila sehemu fulani,iwe kufukuzwa
kazi,kudhurumiwa,kutendewa mabaya na watu tuliowaamini lakini
wakageuka,bado Mungu atafungua kwa njia nyingine. Sisi ni wabarikiwa na ni
kipawa tulichopewa kama biblia isemavyo"kipawa ni kito cha thamani na kila
kigeukapo hufanikiwa,)Maana ya kila kigeukapo inamaanisha kila uendapo na kila
ufanyacho utafanikiwa.Shetani japo alijaribu kugusa maisha ya Ayubu kwa
magonjwa,kuuwa watoto wake na mifugo na mali zake kufilisiiwa,bado alimtegemea
Mungu na matokeo ya mwisho yalikuwa mazuri kuliko mwanzo na alipata utajiri
mwingi kuliko mwanzo.Hata kama shetani alichezea uchumi wako na ukakata
tamaa,nakutia moyo kuwa baraka yako bado ipo si za kubahatisha,Yesu atakubariki
kwani anazo baraka nyingi.Pia baraka zetu zinatufuata popote tunapoenda kama
neno lisemavyo " hakika wema na fadhiri zitatufuata siku zote
za maisha yetu, ZABUR 23:6"
Pia baraka zetu anayetoa ni Mungu na ndie anatupa nguvu za
kupata utajiri( KUMB 8:17:18) Wala si uwezo wetu hivyo tumtegemee
yeye ambae ndiye neno (YOHAN 1:1) Ili atupe mahitaji yetu,
Vitu vyote vipo chini yake na anatoa kwakila mtu anaye
mcha na kumtii( 1MAMB NYKT 29:12).
Ushauri wangu kwako mpe Yesu maisha yako utapata baraka za Bwana ambazo zinajumuishwa na upendo,furaha,na amani kisha utajiri wa fedha,mifugo,mashamba,majumba,magari n.k Bwana atatuzidishia na baraka ya Mungu inaenda hatua kwa hatua,yapasa uwe mvumilivu kama baba yetu Ibrahim aliyepita wakati mgumu lakini mwisho wake ulikuwa mzuri.Usitake utajiri kwa haraka dunia itakupoteza.wengi tunawaona walitaka utajiri kwa haraka lakini wamekufa mapema tena kwa vifo vya kuhuzunisha na pesa na utajiri wao hawakuufaidi bali wamefaidika wengine.Baraka ya Mungu hutajirisha na haichangamani na majuto.Mungu awabariki.
Kwa Msaada Zaidi
Waweza kuwasiliana nami
0688387834
luggymakky@gmail.com
Ushauri wangu kwako mpe Yesu maisha yako utapata baraka za Bwana ambazo zinajumuishwa na upendo,furaha,na amani kisha utajiri wa fedha,mifugo,mashamba,majumba,magari n.k Bwana atatuzidishia na baraka ya Mungu inaenda hatua kwa hatua,yapasa uwe mvumilivu kama baba yetu Ibrahim aliyepita wakati mgumu lakini mwisho wake ulikuwa mzuri.Usitake utajiri kwa haraka dunia itakupoteza.wengi tunawaona walitaka utajiri kwa haraka lakini wamekufa mapema tena kwa vifo vya kuhuzunisha na pesa na utajiri wao hawakuufaidi bali wamefaidika wengine.Baraka ya Mungu hutajirisha na haichangamani na majuto.Mungu awabariki.
Kwa Msaada Zaidi
Waweza kuwasiliana nami
0688387834
luggymakky@gmail.com
Monday, August 4, 2014
Wednesday, July 16, 2014
Tuesday, July 15, 2014
Monday, July 14, 2014
UMUHIMU WA MABADILIKO
Nawasalimu kwa jina kuu la Yesu wasomaji wote wa Blog hii,
napenda kushiriki nanyi kile kilichofundishwa jana katika ibada,Tulipata mgeni kutoka Turiani Morogoro,Mtumishi wa Mungu Joshua Malundo yupo nasi kwa wiki ya pili sasa.
Anaendelea kutuletea yale mungu aliyompa kusema nasi.
Mungu alisema nasi juu ya UMUHIMU WA MABADILIKO,
Msingi wa somo hili ulitoka katika maandiko ya Mungu katika kitabu cha 1Samwel 10:1-7,
Kuna umuhimu mkubwa sana wa sisi kama watu wa Mungu kubadlika na hilo ndilo Mungu anatamani sana kuliona kutoka kwetu.Hata yeye alipotuokoa alitubadilisha kutoka kwenye utu wa kale na kutuvika utu upya.Lakini katika mabadiliko yapo yaliyo mbadiliko sahihi na ambayo si sahihi.
Badiliko linalotka kwa Mungu huwa ni sahihi sikuzote.Hitaji badiliko sahihi katika kila eneo la maisha yako.
Sehemu za picha katika ibada hiyo
| kipindi cha Sifa |
| Sehemu ya kusanyiko |
| Mtumishi wa Mungu akitoa shukrani kwa kupata mtoto salama |
| Mtumishi wa Mungu akimshukuru Mungu baada ya maombi yaliyofanyika kanisani hapa kwa wiki moja,Mungu ameanza kufungua njia katika kazi za mikono yake |
| Mwenyekiti msaidizi wa ujenzi wa Hekalu la Mungu,naye alimshukuru Mungu kwa kumponya mguu wake uliovunjika wiki mbili zilizopita |
| Baraka kutoka kwa Mchungaji |
| Kwa Mungu wote ni vijana akimwimbia Mungu |
| Mtumishi wa Mungu Teddy Komba |
| Praise Team |
| Tutamsifu Mungu kwa kila hali |
| Mwinjilisti Joshua Malundo akifundisha |
| Wakati wa Maombezi |
| Darasa la watoto |
Saturday, July 5, 2014
SIKU 7 ZA MAOMBI YA KUFUNGA NA MKESHA ZAKARIBIA KUMALIZIKA
Ni neema nyingine ambayo Mungu Mwenye enzi ametupatia Paradise,
Mungu alisema na Mtumishi Wake Mchungaji Kiongozi Lugano Mwakisole juu ya maombi ya siku 7 kwa kanisa na juu ya ujenzi wa hema yake.
Maombi hayo yalianza Tar 30/06/2014 na yatamalizika tar 6/07/2014 Usiku.
Mungu ni wa ajabu sana kupitia maombi hayo kuna mambo mengi Mungu amefanya kwa mtu mmoja mmoja na kwa kanisa kwa ujumla.Tunaendelea kumtukuza Mungu maana ameonekana Paradise.
Hizi ni sehemu za Picha za wanajeshi wa Yesu walioshiriki katika mkesha huo.
Mungu alisema na Mtumishi Wake Mchungaji Kiongozi Lugano Mwakisole juu ya maombi ya siku 7 kwa kanisa na juu ya ujenzi wa hema yake.
Maombi hayo yalianza Tar 30/06/2014 na yatamalizika tar 6/07/2014 Usiku.
Mungu ni wa ajabu sana kupitia maombi hayo kuna mambo mengi Mungu amefanya kwa mtu mmoja mmoja na kwa kanisa kwa ujumla.Tunaendelea kumtukuza Mungu maana ameonekana Paradise.
Hizi ni sehemu za Picha za wanajeshi wa Yesu walioshiriki katika mkesha huo.